ATLETICO MADRID-MARTINEZ:

Atletico Madrid imefanikiwa kumsajili mshambuliaji wa Porto Jackson Martinez kwa dau la euro milioni 35, baada ya kumkosa kwa mshambuliaji wa Juventus Carlos Tevez.
MANCHESTER UTD-BOATENG:

Louis van Gaal ana nia ya kumsajili beki wa kati wa klabu ya Bayern Munich Jerome Boateng. Manchester United wamejiandaa kutoa dau la euro milioni 28 kwa ajili ya kumpata mchezaji huyo raia wa Ujerumani.
LIVERPOOL-BACCA:

Klabu ya Sevilla imeiambia klabu ya Liverpool kwamba mchezaji wao Carlos Bacca ataigharimu klabu hiyo pauni milioni 21. Mchezaji huyo aliyefanya vema katika mshindano ya Ligi ya Europa anasakwa na kocha wa Liverpool Brendan Rodgers ila atatua Liverpool kama watafikia dau lake la uhamisho.
AC MILAN-VAN PERSIE:

AC Milan wana hamu kubwa ya kumsajili mshambuliaji mwenye jina kubwa msimu huu na inaweza kuingia kwenye mbio za kumuwania mshambuliaji wa Manchaster United Robin van Persie ambaye ameonesha nia ya kutimka klabuni hapo.
MANCHESTER UTD-LUCAS BIGLIA:

Meneja wa Manchester United Louis van Gaal ametuma maskauti katika klabu ya Lazio ili kumtazama Lucas Biglia lakini Mholanzi huyo hana nia tena na kiungo huyo mwenye umri wa miaka 29.
MANCHESTER CITY-GERONIMO RULLI:

Klabu ya Manchester City wana nia ya kumsajili mlinda mlango wa Real Sociedad Geronimo Rulli, lakini watamtoa kwa mkopo katika klabu ya Valencia.
CHELSEA-ALEX SONG:

Klabu ya Chelsea imeipiku klabu ya West Ham katika mbio za kuiwania saini ya kiungo wa klabu ya Barcelona Alex Song. Mchezaji huyo ana thamani ya pauni 5 milioni.
ARSENAL-JOEL CAMPBELL:

Arsenal inatazamia kumuuza mchezaji wake Joel Campbell msimu huu na imefumgua milango kwa ofa ya pauni milioni 5, Fenerbahce na Real Sociedad ni miongoni mwa klabu zinazomuhitaji mshambuliaji huyo.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
ARSENAL YAANGUKIA PUA KWA MARTINEZ ATUA ATLETICO MADRID, MAN UTD YAMUWANIA JEROME BOATENG, CHELSEA YAONGOZA MBIO KUMNASA ALEX SONG...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment