
Klabu ya Real Madrid imesema kwamba kama beki wake wa kati Sergio Ramos atatimka klabuni hapo basi itafanya juu chini kumpata mlinzi wa kati wa klabu ya Arsenal Laurent Koscielny kwa ada ya pauni milioni 21.5.
Kwa mujibu wa France Football, Laurent Koscielny aliongeza mkataba mpya na klabu ya Arsenal msimu uliopita, ametakiwa na kocha wa klabu ya Real Madrid Rafa Benitez kama mchezaji ambaye ataimarisha safu ya ulinzi wa kikosi chake baada ya Sergio Ramos kuondoka klabuni hapo.
Inaaminika kwamba mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania ameomba kutimka klabuni hapo na kujiunga na Manchester United baada ya matakwa yake kushindwa kufikiwa.

Pepe na Raphael Varane wamehusishwa pia katika tetesi za kutimka klabuni hapo, huku klabu ya Chelsea ikimfuatilia Varane kwa ukaribu zaidi.
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger yupo katika wakati mgumu kwa sasa wa kuwabakiza wachezaji nyota katika kikosi chake kwa ajili ya kuwania mataji msimu ujao.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
BAADA YA VERMAELEN KUJIUNGA BARCELONA, REAL MADRID WAGONGA HODI ARSENAL...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment