Dylan Kerr wa Simba, Donald Ngoma na James Zutah wa Yanga wawasili nchini tayari kwa kumaliza taratibu nakuanza vibarua vyao vipya
Donald Ngoma na James Zutah wa Yanga wawasili nchini

WACHEZAJI wapya wa Yanga, Donald Ngoma na kiungo raia wa Ghana James Zutah wamewasili nchini Jumamosi kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kujiunga na mabingwa hao wa msimu uliopita.
Katibu wa Yanga Dk Jonas Tiboroha ameiambia Goal kuwa zoezi la kwanza litakuwa ni kuwapima afya zao, kisha masuala ya kumalizana nao kimkataba yatafuatia wakati wowote.
Wamekuja kwa ndege ya KQ kwa wakati mmoja na kupokelewa na katibu Dk Tiboroha, katabaro na Ndama.
Kiungo James amekuja kuchukua nafasi ya Lansana Kamara aliyeshindwa kumridhisha kocha Hans van der Pluijm.
Dylan Kerr wa Simba awasili nchini
Kocha Mkuu mpya wa Klabu ya Simba, Muingereza Dylan Kerr amewasili nchini Jumamosi akiwa sambamba na kocha wa makipa raia wa Kenya Abdul Iddi Salim.
Kerr ameiambia Goal amekuja nchini kuanza kazi na anamatumaini makubwa atafanya viuri kutokana na kulijua vyema soka la Afrika.
Amesema anajua Simba ni timu kumbwa Tanzania na atajitahidi kutoa kila alichokuwa nacho ili kuipa mafanikio timu hiyo iliyomaliza nafai ya tatu msimu uliopita.
Kerr ametua nchini kuchukua nafasi ya Goran Kopunovic aliyeshindwa na uongozi wa Simba kuhusu maslahi yake ya kuongeza mkataba mpya.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
Dylan Kerr wa Simba, Donald Ngoma na James Zutah wa Yanga wawasili nchini...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment