CHELSEA:

Mshambuliaji wa Monaco na timu ya taifa ya Colombia Radamel Falcao amejiunga na mabigwa wa ligi kuu Uingereza Chelsea baada ya kukubaliana na miamba hao kuhusu masharti ya mkataba siku ya Jumamosi.
MANCHESTER CITY:

klabu ya Manchester City iliyoshikilia nafasi ya pili ligi kuu Uingereza msimu ulioisha 2014/2015, in nia ya kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Real Madrid Angel Di Maria anayekipiga Manchester United. Txiki Begiristain amewaomba wawakilishi wa mchezaji huyo kuzungumza nae kama atakuwa tayari kujiunga na Man City kutoka Man Utd.
ARSENAL:

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameamua kuelekeza nguvu zake kwa kiungo wa Bayer Leverkusen Lars Bender mwenye thamani ya pauni milioni 18.
MANCHESTER UNITED:

Mshambuliaji wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Manchester United Wayne Rooney amemsihi kocha wake Louis van Gaal kumleta mshambuliaji mwenzake wa timu ya taifa na klabu ya Tottenham Harry Kane. Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Uingereza anaamini kuwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 21 atafanikiwa zaidi kama akijiunga na klabu hiyo yenye makazi yake mjini Manchester. Harry Kane anasadikika kuwa na thamani ya pauni milioni 40.
LIVERPOOL:

Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers anaongoza katika mbio za kuwania saini ya mshambuliaji wa klabu ya QPR Charlie Austin. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 anasakwa pia na klabu ya Newcastle United.
REAL MADRID:

Klabu ya Real Madrid ipo tayari kumuuza Iker Casillas ambaye anaweza kujiunga na mahasimu wa Arsenal klabu ya Tottenham. Kipa wa Tottenham Hugo Lloris anatazamiwa kuwa mbadala wa kudumu wa golikipa wa Manchester United David De Gea.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
FALCAO ATUA CHELSEA, MAN CITY YAMTAKA DI MARIA ETIHAD, MADRID KUMUUZA CASILLAS SPURS....
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment