
Santi Cazorla ameondoa hofu iliyokuwa imetanda kwa mashabiki wa Arsenal kuhusiana na mchezaji huyo kutimka klabuni hapo kujiunga na klabu ya Hispania Atletico Madrid lakini Santi amesema hawezi kutimka Arsenal. Cazorla amesema ana furaha Arsenal na wala hana mpango wa kuondoka.
"Tetesi kuhusiana na Atletico Madrid ni za uongo. Kwasasa, mawazo yangu yapo Arsenal. Nina miaka wiwili iliyobakia kwenye mkataba wangu na nina imani nitaimaliza," kiungo huyo aliimbia Goal.
"Nina furaha sana Arsenal na Ligi hii pia. Nahisi kupendwa na kuthaminiwa na timu pamoja mashabiki."
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 alikuwa ni chaguo la Arsene Wenger katika nafasi ya kiungo msimu uliopita na pia kama mchezaji wa msimu wa klabu hiyo.
"Sifahamu kama msimu huu ulikuwa bora sana katika maisha yangu ya soka lakini nimejisikia vizuri kuwa na timu hii, kucheza katika nafasi mpya ambayo huwa najisikia vizuri nikicheza," Cazorla aliongezea. "Nina tumai nitakuwa bora zaidi msimu ujao.
"Kama tunahitaji kuchukuwa ubingwa wa ligi, ni lazima kudumisha kiwango kama tulivyokuwa katika mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Nadhani kuwa tunahitaji kapigana na klabu za Chelsea, Manchester Utd, na Manchester City, watakuwa imara zaidi msimu ujao.
"Tunafuraha kushinda kombe la FA tena, ni muhimu sana kwa sisi kushinda mataji na sasa tunajiandaa vema na msimu ujao. Tunataka kufika hatua ya juu zaidi katika ubora wetu na nina matumaini tutapigania Ligi Kuu na kwenda zaidi katika Ligi ya Mabingwa."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
HABARI NJEMA KWA MASHABIKI WA ARSENAL...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment