
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Argentina Carlos Tevez amesema kwamba mtu yeyote asiyemkubali mchezaji mwenzake Lionel Messi hajui lolote kuhusu mpira.
Leo saa sita usiku timu ya taifa Argentina itamenyana vikali dhidi ya timu ya taifa ya Paraguay katika mashindano ya Copa America kundi B, na Messi akitegemewa kuwa mchezaji kivutio katika michuano hiyo huku mchezaji mwanzake Tevez akitegemea kuanzia benchi katika mchezo huo.
Mshambliaji huyo wa Barcelona na mshindi wa tuzo za Ballon d'Or mara nne, alikiongoza kikosi hicho cha Argentina katika mashindano ya kombe la dunia na kufikia hatua ya fainali huku mchezaji mwenzake Tevez akiachwa na aliyekuwa kocha wa timu hiyo Alejandro Sabella.
Hata hivyo, Carlos Tevez anabakia kuwa mchezaji maarufu zaidi ya Lionel Messi nchini kwao Argentina huku akisifika zaidi kama "Mchezaji wa Watu."

Lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 anasema Messi anahitaji kupewa heshima ya kipekee kutoka kwa mashabiki wa taifa hilo.
"Naamini watu wanampenda Messi kwasababu ni Muargentina na ni bora zaidi duniani," Tevez aliiambia tovuti rasmi ya Copa Amerika katika mahujiano.
"Yeyote asiyempenda Messi hajui chochote kuhusu mpira na sijui ni nini anawaza katika kichwa chake," aliongezea.

Tevez anajichukulia kama mchezaji mzuri tangu kushuka kwa kiwango chake miaka ya karibuni na anaamini Messi ana nufaika kwa kupungua uzito hivi karibuni.
"Nina upungufu wa kilo 8," alisema. "Ninafikiri nipo vizuri kiumbo, kihisia na kimchezo. Nipo bora zaidi ya nilivyokuwa zamani."
"Messi hajabadilika. Ila kilichobadilika ni kwamba amepunguza kilo tatu au nne tofauti na zamani. Hii inamaanisha ana ari zaidi, inabadilisha akili yako, inabadilisha kila kitu."
"Naamini huu ni wakati wake kwa sasa."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
"HUMPENDI MESSI?, HUJUI LOLOTE KUHUSU MPIRA"-TEVEZ
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment