"KUWA NA MCHEZAJI KAMA FIRMINO NI SAWA NA KUWA NA LULU MKONONI"-RONADINHO GAUCHO.

Thursday, 25 June 2015



Mkongwe wa Brazili Ronadinho Gaucho anaamini kuwa klabu ya Liverpool imepata suluhisho la ukame wa magoli klabuni hapo.

Bosi wa Liverpool Brendan Rogders anaamini kuwa mchanganyiko wa Samba ya Coutinho na Firmino ambaye amesajiliwa hivi karibuni utaongeza msisimko katika uwanja wa Anfield msimu ujao.

Huku klabu ikiendelea kumfukuzia mshambuliaji wa Sevilla Carlos Bacca- na huku wakimngojea mshambuliaji wao Daniel Sturridge ambaye yupo nje kwa majeruhi, Ronadinho anaamini ya kuwa klabu ya Liverpool haitakuwa na la kujitetea kama hawataimarika kutokana na kuwa na magoli machache msimu uliopita.

Daniel Sturridge (Liverpool)

Mshindi huyo wa kombe la dunia mwaka 2002 alisema, "Ni mafanikio makubwa kwa Liverpool kuwapata Coutinho na Firmino. Itawapa moja kati ya viungo matata barani Ulaya. Ubunifu, akili na malengo waliyonayo kati yao itaibadilisha Liverpool kama timu kwa ujumla. Kuwa na viungo kama hao wawili kunawapa nafasi kubwa ya kufuzu katika Ligi ya Mabingwa msimu ujao.

"Ni ndoto kwa washambuliaji wa Liverpool kuwa na huduma kama hiyo. Kama huwezi kufunga magoli katika timu ukiwa na viungo kama Coutinho na Firmino, huwezi kufunga katika timu nyingine yoyote. Watatengeneza nafasi nyingi."

Ronaldinho smiles

Firmino mwenye umri wa miaka 23 ni habari nyingine katika soka, ametundika magoli 49 katika mechi 153 akiwa katika klabu ya Hoffenheim. Mchezaji huyo mwenye thamani ya euro milioni 28 ameisaidia nchi yake kufikia hatua ya robo fainali, akifunga goli dhidi ya Venezuela.

Anauwezo wa kucheza nafasi tofauti tofauti uwanjani. Ingawa alianza michuano akiwa na Hoffenheim kama kiungo wa kati mshambuliaji, Firmino anaweza kucheza nafasi zote za pembeni na pia kama mshambuliaji wa kati-akiwa ameshaifanyia hivyo nchi yake.

0 comments:

Post a Comment