MANCHESTER UNITED - SERGIO RAMOS

Manchester United wemeripotiwa kutenga dau la euro milioni 40(€40m) katika jitihada za kumsajili beki wa Real madrid Sergio Ramos.
ARSENAL - FAOUZI GHOULAM

Arsenal wanajiandaaa kuipatia Napoli £9m kwa ajili ya Faouzi Ghoulam wiki hii. Beki huyo wa kushoto mwenye umri wa miaka 24 pia amekuwa akiwaniwa na klabu ya Chelsea na Manchester City, lakini Arsenal wamevutiwa na mchezaji huyo na kuanza kuitafuta saini yake.
CHELSEA - ASMIR BEGOVIC & JOHN STONES

Ofa ya Chelsea ya pound milioni 6(£6m) imekataliwa na klabu ya Stoke City kwa ajili ya kumsajili golikipa Asmir Begovic ambaye anatarajiwa kuwa mrithi wa Petr Cech. Potters wanahitaji pound milioni 10(£10m) kwa ajili ya golikipa huyo mwenye umri wa miaka 28.

Chelsea wanajiandaa kumsajili beki wa Everton John Stones. Kijana huyo wa Toffees kwa sasa thamani yake inasadikiwa kuwa £20m.
BARCELONA,CHELSEA,MANCHESTER CITY - PAUL POGBA

Juventus imepokea Ofa tatu kutoka Barcelona waliokuwa wametoa €80m pamoja na €10m kama nyongeza kutokana na thamani ya Paul Pogba, ambaye anatarajia kujiunga na mabingwa hao wa UEFA msimu ujao. Chelsea wakaweka €50m pamoja na Oscar kwa matumaini ya kumpata mchezaji huyo haraka iwezekanavyo, pia Manchester City wakaweka ofa ya € 100m kwa ajili ya kiungo huyo.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MANCHESTER UNITED YATOA €40M KWA RAMOS,FAOUZI GHOULAM KUTUA ARSENAL,OFA YA CHELSEA YAKATALIWA,POGBA AWEKEWA OFA TATU........
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment