
Meneja wa Chelsea Jose Mourinho anasema "Inamuuma" kuona watu wa soka la Kiingereza hawajashuhudia makali ya mshambuliaji mahili wa kimataifa wa Colombia Radamel Falcao, na hivyo ana mpango wa kumsaidia mchezaji huyo kurudisha makali yake katika kuzitingisha nyavu za wapinzani.
Radamel Falcao alijiunga na klabu ya Manchester United kwa mkopo msimu uliokwisha akitokea klabu ya Monaco lakini tangu ajiunge na klabu hiyo hajaonesha makali kama ilivyotegemewa na hivyo klabu hiyo ina mpango wa kuachana naye.
Jose Mourinho ametoa fursa ya kumsaidia mchezaji huyo kurudi katika kiwango chake cha awali kama atajiunga na klabu ya Chelsea iliyotwaa Ubingwa wa Ligi msimu ulioisha.
Mtandao wa Goal ulitoa taarifa mwanzoni mwa mwezi Juni kwamba Mourinho amekuwa msukumo mkubwa katika klabu hiyo kuhusiana na Falcao kujiunga na miamba hao akiwa na imani ya kurejesha kiwango cha mshambuliaji huyo kama alivyokuwa katika klabu za Porto ya Ureno na Atletico Madrid ya Hispania.
Sasa Kocha huyo Jose Mourinho ameuthibitishia umma kupitia DirecTv Sports kwamba,"Ni kweli inauma sana kwamba watu nchini Uingereza wanaamini kwamba waliyemuona Manchester United ndiye Falcao"
"Ni mchezaji ninayemfahamu, mchezaji ambaye nimekuwa nikimfuatilia tangu akiwa na klabu ya Atletico Madrid na kama ninaweza kumsaidia Falcao kurudi katika ubora wake nitafanya hivyo."
Falcao ana nia ya kuendelea kubaki na kukipiga katika ligi hiyo bora barani Ulaya na anataka kujiunga na Mourinho Stamford Bridge baada ya kutimka Manchester United.
Baada ya mshambuliaji huyo kushindwa kuwika mbele ya kocha Louis Van Gaal, klabu ya Manchester United haikutaka tena kuchukua uamuzi wa kumnunua mchezaji huyo aliyekuwa klabuni hapo kwa mkopo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 aliifungia klabu hiyo jumla ya magoli manne tu katika michezo 26 ya ligi kuu aliyoshiriki na iliripotiwa kwamba uhusiano wake na kocha Van Gaal katikati ya msimu haukuwa mzuri.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MOURINHO: MLIYEMUONA MAN UTD SIO RADAMEL FALCAO
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment