
Mshikemshike wa uchaguzi wa viongozi wa klabu ya Coastal Union tayari umeshaanza mara baada ya kamati ya uchaguzi ya TFF kufanya mchujo wa awali wa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi kwenye klabu hiyo ya Wagosi wa Kaya ya jijini Tanga.
Wagombea watano wa nafasi ya ujumbe na mgombea mmoja wa nafasi ya uenyekiti wameondolewa katika kinyang’anyiro hicho baada ya kukosa sifa ya kuwa na elimu ya kidato cha nne kutokana na kutoambatanisha vyeti vyao vya elimu hiyo vinavyotambuli wa baraza la mitihani la taifa NECTA.
Hussein Abdul Ally aliyekuwa anagombea nafasi ya makamu mwenyekiti, ameondolewa kwasababu ya kukosa cheti cha elimu ya kidato cha nne. Wagombea wengine ambao wameondolewa kwa kukosa sifa hiyo ni pamoja na Hussein Ally Mwinyihewa, Omary Mwambashi, Mohamed Ally Mohamed maarufu kama ‘Dondo’ wakati Salumu Pelembe yeye hana uthibitisho wowote kwenye fomu zake hivyo kamati ya uchaguzi ya TFF kuamua kuliondoa jina lake.
Wagombea waliopitishwa kwa upande wa nafasi ya mwenyekiti ni Dkt. Ahmed Ally Twaha na mzee Steven Mguto ambaye pia alishawahi kupitishwa, lakini ametakiwa apeleke barua ya uthibitisho wa elimu yake kutoka baraza la mitihani la taifa NECTA.
Kwa upande wa makamu wa mwenyekiti, Salim Amir Fakki ndiye mgombea pekee aliyepitishwa kuwania nafasi hiyo baada ya wagombea wengine kuenguliwa kwasababu ya kutotimiza vigezo.
TFF itaanza kupokea mapingamizi yote kwenye ofisi zake jijini Dar es Salaam au wamkabidhi mjumbe wa kamati ya TFF kanda ya Tanga na Kilimanjaro Halid Abdallah ili aweze kuyatuma mapingamizi kupita baruapepe ya katibu mkuu wa TFF au ile ya TFF kabla ya Juni 13 mwaka huu. Juni 13 kamati ya uchaguzi itakuwepo jijini Tanga kupitia pingamizi kama zipo, Juni 14 itakuwa ni siku ya usahili kujua nani amepita na nani ameondolewa kabla ya kuelekea kwenye hatua ya uchaguzi.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
SAKATA LA UCHAGUZI WA VIONGOZI COASTAL UNION
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment