
Kufuatia kutangazwa kwa ratiba ya Ligi Kuu msimu ujao, tovuti ya Goal imetoa takwimu mbali mbali kuhusiana na mechi za ufunguzi.

1. Wayne Rooney amefunga magoli sita katika mechi za ufunguzi mwishoni mwa wiki zaidi ya mchezaji mwingine yeyote wa Ligi Kuu wa sasa.

2. Arsenal waneoneshwa kadi nyekundu nyingi siku ya ufunguzi, kadi sita zaidi ya timu yoyote ya Ligi Kuu.

3. Wachezaji saba wamefunga mabao matatu "Hat-Trick" siku ya mechi za ufunguzi-Mick Quinn (1993) , Mathayo Le Tissier (1995) , Kevin Campbell (1996) , Fabrizio Ravanelli (1996) , Dion Dublin (1997) , Gabby Agbonlahor (2008) na Didier Drogba (2010) .

4. Kulinganisha na wapinzani wao wa jadi Arsenal wenye wastani wa 1.96, Tottenham wana wastani wa 1.36 tu katika mechi za ufunguzi mwishoni mwa wiki.

5. West Ham wamepoteza mechi nyingi za ufunguzi wa Ligi Kuu zaidi ya timu nyingine yoyote.

6. Swansea wamefunga magoli mengi katika mechi zao za ufunguzi misimu mitatu iliyopita (8), kama walivyofanya kwenye jumla ya michezo yao tisa iliyopita.

7. Newcastle United imeshindwa kufunga mechi nne za ufunguzi kwa misimu mitano, lakini imekutanishwa na Manchester City (Mara Mbili), Arsenal, na Manchester United, na imeweza kuifunga Tottenham pekee katika mechi hizo.

8. Liverpool imetoa sare ya bila kufungana mara tatu katika mechi za ufunguzi wa Ligi Kuu (1992-1993 , 2005-06 , na 2012-13).
9. Bournemouth wameshinda michezo yao miwili ya ufunguzi wa ligi, baada ya kufanikiwa kupata ushindi mmoja kati ya mechi zao 13 zilizopita, wametoa sare mechi sita na kupoteza mechi sita.
10. Chelsea wameshinda michezo 14 bila kupoteza mchezo wowote kati ya 16 waliyocheza mwisho wa wiki wa ufunguzi wa ligi. The Blues hawajapoteza mchezo wowote wa ufunguzi wa ligi tangu msimu wa 1998-99 walipopigwa na Coventry City.
11.Everton imeruhusu magoli mengi katika mechi za ufunguzi za kila mwisho wa wiki zaidi ya timu nyingine yoyote. Imefungwa magoli 35.
12. Manchester United ni timu pekee iliyopoteza mechi ya ufunguzi za mwishoni mwa wiki lakini mbele iliendelea kufanya vizuri na kunyakuwa ubingwa, imefanya hivyo misimu ya 1992-1993 , 1995-1996 na 2012-13.
13. Manchester City imeshinda michezo mitano ya mechi za ufunguzi katika misimu sita, imetoa sare mchezo mmoja. Mechi mbili mfululizo imeshinda dhidi ya Newcastle United.

14. Stoke City imeshinda mara moja katika michezo yake ya ufunguzi ya Ligi Kuu-dhidi ya Burnley 2009-10.
15. Magoli mengi yaliyoshuhudiwa katika michezo ya ufunguzi wa msimu ni 36 ya msimu wa 2003-04. Huku Manchester United ikiongoza kwa kuichapa Bolton 4-0.
16. Katika misimu miwili iliyopita, wote Fulham na Hull City wameshinda michezo yao ya ufunguzi wa Ligi Kuu.
17. Mchezo wa mwisho Watford kupoteza mwanzoni mwa msimu ulikuwa msimu wa 2006-07 dhidi ya Everton, walikuwa Ligi Kuu wakati huo.
18. Southampton wametoa sare mechi zao za ugenini za ufunguzi wa ligi katika misimu mitano iliyopita. Wameshinda mmoja, wametoa sare moja, wamepoteza tatu.

19. Arsenal imepoteza mchezo mmoja tu kati ya michezo 14 ya ufunguzi wa Ligi Kuu. Imeshinda tisa, imetoa sare michezo minne.
20. Manchester United kufungwa nyumbani Old Trafford na Swansea City msimu uliopita ilikuwa ni mara ya kwanza tangu msimu wa mwaka 1972-73.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
TAKWIMU MBALIMBALI ZA MECHI ZA MWANZO LIGI KUU UINGEREZA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment