
Klabu ya Chelsea na Monaco zimekubaliana vigezo vya uhamisho wa mkopo wa mshambuliaji Radamel Falcao.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia ambaye alisajiliwa kwa ada ya pauni milioni 50 kutoka Ligue 1 mwaka 2013, atakaa na klabu ya chelsea kwa msimu wa 2015-2016.
Kiungo chipukizi wa Chelsea Mario Pasalic, mwenye umri wa miaka 20 atajiunga na klabu ya Monaco kwa mkopo kama sehemu ya makubaliano yao.
"Nina furaha sana kujiunga na Chelsea na siwezi kusubiri kuanza mazoezi na kutoa msaada katika kusudio letu la kuulinda ubingwa wa Ligi na kuwa na mafanikio Ulaya." Falcao aliiambia tovuti rasmi ya klabu.
Goal ilitanabaisha mwezi uliopita kwamba Jose Mourinho alikuwa akitoa msukumo kwa Chelsea kumuwania Falcao, ambaye ana mpango wa kuamsha makali yake katika ngazi ya juu baada ya kuwa na msimu mbovu pale Manchester United.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alifunga magoli tisa katika michezo kumi na saba ya msimu wa kwanza akiwa na Monaco lakini kampeni yake iliisha baada ya kukumbwa na majeraha yaliyomfanya akose kushiriki kombe la Dunia mwaka jana.
Baadae Falcao alijiunga na klabu ya Manchester United kwa mkopo siku ya mwisho ya dirisha la usajili mwaka jana lakini amefurukuta kufanya vema Old Trafford bila mafanikio yoyote, alifunga magoli 4 kwenye michezo 29 aliyoichezea klabu hiyo.
Kabla ya kujiunga na klabu ya Monaco, Falcao alitambulika kama mshambuliaji matata na hatari baada ya kufunga magoli 70 katika misimu miwili tu akiwa na klabu ya Atletico Madrid na kutupia magoli matatu "Hat-trick" kwenye mechi ya Super Cup mwaka 2012 dhidi ya Chelsea.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
BAADA YA KUIGALAGAZA CHELSEA MWAKA 2012, SASA ATUA RASMI KLABUNI HAPO...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment