CHELSEA - FALCAO

Radamel Falcao amekubali kujiunga kwa mkopo na klabu ya Chelsea na uhamisho wa mchezaji huyo kutoka Monaco umepangwa kukamilika wiki ijayo. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia aliambiwa ahudhurie kwenye mazoezi na Blues kwa ajili ya kujianda na msimu ujao.
UNITED - ARDA TURAN

Arda Turan ameikacha ofa ya Manchester United ya £29m kwani moyo wa mchezaji huyo unatamani kucheza chini ya kocha wa Chelsea Jose Mourinho. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uturuki anatarajia kuihama Atletico Madrid baada ya klabu hiyo kukubali kupokea ofa ya mchezaji huyo.
BARCELONA - ARDA TURAN

Barcelona wapo kwenye mstari wa mbele kukubaliana na Arda Turan na wasaidizi wake. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uturuki anataka kuondoka Atletico Madrid na usajili wake kwenda Camp Nou unaweka ukawa wazi wiki hii.
MANCHESTER CITY - KEVIN DE BRUYNE

Manchester City hawajakata tamaaa juu ya kumsajiri mchezaji wa Wolfsburg Kevin De Bruyne, licha ya kuuambiwa kwamba hauzwi. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji ana thaman ya £35m lakini mchezaji huyo hajasaini mkataba mpya na klabu yake ya sasa.
EVERTON - SAM BYRAN

Everton tayari wameamua tafuta mbadala wa Seamus Coleman baada ya Manchester United kuonyesha nia ya kumnyakua beki huyo. Toffees wamepanga kumsajiri mchezaji wa Leeds United Sam Byram kama beki huyo ataondoka.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
FALCAO AELEKEA CHELSEA RASMI,TURAN AITOSA MANCHESTER UNITED,EVERTON YAMPATA MBADALA WA COLEMAN,MANCHESTER CITY WARUDI KWA KEVIN.....
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment