"NITATIMKA MAN UTD, NIKATULIE NA MKE WANGU"-VAN GAAL...

Tuesday, 28 July 2015



Meneja wa Manchester United Louis Van Gaal amesema kuwa huenda akaondoka katika kilabu cha Manchester United mwisho wa kandarasi yake ya miaka mitatu ili kutimiza ahadi alioitoa kwa mkewe.

Alipoulizwa iwapo ataongeza kandarasi yake katika uwanja wa Old Traford ,raia huyo wa Uholanzi ameiambia BBC kwamba ataondoka mwisho wa kandarasi yake mwaka 2017.

"Nilimuahidi mkewe wangu, hatuna miaka mingi iliosalia, na hiyo ndio sababu," alisema meneja huyo mwenye umri wa miaka 63.

"Nimefanya kila kitu katika maisha yangu kama mkufunzi." Alipoulizwa iwapo kuna uwezekano wa yeye kusalia katika kilabu hicho, alijibu kwamba hawezi kutoa jibu lolote kwa kuwa mkewe amekasirika sana.

"Nakiri kwamba nilimwambia kuwa nitaastaafu ifikiapo miaka 55 lakini nikiwa na miaka 63 bado naendelea na ukufunzi na wiki ijayo nitakuwa na miaka 64," alisema meneja huyo.

0 comments:

Post a Comment