
Meneja wa Manchester United Louis Van Gaal amesema kuwa huenda akaondoka katika kilabu cha Manchester United mwisho wa kandarasi yake ya miaka mitatu ili kutimiza ahadi alioitoa kwa mkewe.
Alipoulizwa iwapo ataongeza kandarasi yake katika uwanja wa Old Traford ,raia huyo wa Uholanzi ameiambia BBC kwamba ataondoka mwisho wa kandarasi yake mwaka 2017.
"Nilimuahidi mkewe wangu, hatuna miaka mingi iliosalia, na hiyo ndio sababu," alisema meneja huyo mwenye umri wa miaka 63.
"Nimefanya kila kitu katika maisha yangu kama mkufunzi." Alipoulizwa iwapo kuna uwezekano wa yeye kusalia katika kilabu hicho, alijibu kwamba hawezi kutoa jibu lolote kwa kuwa mkewe amekasirika sana.
"Nakiri kwamba nilimwambia kuwa nitaastaafu ifikiapo miaka 55 lakini nikiwa na miaka 63 bado naendelea na ukufunzi na wiki ijayo nitakuwa na miaka 64," alisema meneja huyo.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
"NITATIMKA MAN UTD, NIKATULIE NA MKE WANGU"-VAN GAAL...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment