MANCHESTER UNITED - RAMOS,SCHWEINSTEIGER,SCHNEIDER & DE GEA

Manchester United imepanga kumpa mkataba wa miaka mitano Sergio Ramos wenye thamani ya €55m (£39m) ukitoa kodi,mchezaji huyo wa kimataifa wa Hisapania hayupo tayari kubaki Bernabeu.

Manchester United wataikosa huduma ya Bastian Schweinsteiger kwani mchezaji huyo anatarajia kukaa katika klabu yake ya Bayern mpaka mkataba wake utakapoisha 2016.

Ofa ya £20 iliyokuwa imetolewa na Manchester United kwa Morgan Schneiderlin imepigwa chini na Southampton.

Manchester United hawajapokea ofa yeyote kutoka Real Madrid kwa ajili ya David De Gea na bado wamesimamia €50m (£35.4m) kwa ajili ya golikipa huyo.
REAL MADRID - FERNANDO LLORENTE

Bosi wa Real Madrid Rafa Benitez anatarajia kumsajili Fernando Llorente ambaye anatarajia kuihama klabu yake ya Juventus msimu huu, mchezaji huyo anahitaji kujiimalisha na kubaki na ubora wake.
BARCELONA - ARDA TURAN

Barcelona wamejipanga kufanya usajili wa nguvu msimu huu, baada ya kufikia makubaliano ya €35m pamoja na motisha kwa nyota wa Atletico Madrid Arda Turan.
Barcelona watakuwa wameipiku klabu ya chelsea ambayo awali ilitangaza kutoa £29(€40.9) bila kuweka motisha kwa mchezaji huyo.
CHELSEA - LOIC REMY & ASMIR BEGOVIC

Chelsea wameamua kuachana na mpango wa kumuuza mshambuliaji Loic Remy msimu huu. West Ham walikuwa wanaongoza mbio za kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa kwa ada ya £15m lakini Jose Mourinho ameonyesha kumhitaji mchezaji huyo.

Jose Mourinho ameongeza dau kwa ajili ya kumsajili golikipa wa Stoke City Asmir Begovic, golikipa huyo ataigharimu Chelsea ada inayosadikiwa kuwa £8. mchezaji huyo wa kimataifa wa Bosnia anatamani kuelekea Stamford Bridge.
MANCHESTER CITY - KEVIN DE BRUYNE & KARIM BELLARABI

Klabu ya Manchester City imekalibia kumnyakua Kevin De Bruyne na watakutana na wakala wa kiungo huyo wiki ijayo.

Manchester City wamejipanga kutoa kitita cha €35 kwa ajili ya winga wa Bayer Leverkusen Karim Bellarabi.
AC MILAN & INTER - MARIO SUAREZ & MATIJA NASTASIC

AC Milan na Inter wapo kwenye mbio za kumsajili kiungo wa Atletico Madrid Mario Suarez.

AC Milan wameamua kumfungia kazi upya beki wa kati wa Schalke Matija Nastasic.
JUVENTUS - OSCAR

Juventus wako tayari kutumia €28(£19.8m) kwa ajili ya kumsajili Oscar kutoka Chelsea.
ATLETICO MADRID - JUAN CUADRADO,MIRALEM PJANIC & FILIPE LUIS

Atletico Madrid wamejiunga na Inter pamoja na Juventus katika mbio za kumnyakua winga wa Chelsea Juan Cuadrado.

Klabu ya Atletico Madrid imepania kunasa saini ya Miralem Pjanic, lakini hawajafikia dau ambalo klabu yake ya Roma imafikia ambayo ni €45m kwa ajili ya kiungo huyo.

Chelsea wameitaka klabu ya Atletico Madrid kulipa €20 kwa ajili ya Filipe Luis
PSG - DI MARIA & PEDRO RODRIGUEZ

klabu ya PSG inatarajia kutoa kitita cha €60m kwa ajili ya winga wa Manchester United Angel Di Maria. Ofa hiyo inatarajiwa kutolewa leo.

Pia klabu hiyo wanaangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Barcelona Pedro Rodriguez
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
RAMOS KUPEWA MIAKA MITANO UNITED,TURAN KUTUA NOU CAMP,DAU LAPANDA KWA MRITHI WA CECH,PSG WATENGA €60M KWA DI MARIA........NA NYINGINE ZA ULAYA ZILIZOJILI LEO........
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment