TETESI ZA USAJILI: MAN UTD KUTOA EURO 100M KWA MULLER, MOUTINHO ARUHUSIWA KUJIUNGA NA ARSENAL...

Thursday, 23 July 2015

MAN UTD KUTOA EURO MILIONI 100 KWA MULLER:



Mshambuliaji wa 'siri' wa Louis van Gaal ni Thomas Muller. United wapo tayari kutoa dau la euro milioni 100 kumpata nyota huyo wa Bayern Munich.

Chanzo: Bird
Jumatano, 7/22/2015 08:01


MOUTINHO YUPO HURU KUJIUNGA NA ARSENAL:



Mchezaji wa kimataifa wa Ureno Joao Moutinho ameambiwa na klabu yake ya Monaco kwamba yupo huru kufanya mazungumzo ya kuhamia Arsenal. The Gunners wamekuwa wakihusishwa na kuwa na nia kubwa juu ya kiungo huyo na yupo huru kufanya makubaliano kuhamia Londoni kaskazini.

Chanzo: Daily Star
Jumatano, 7/22/2015 15:56

ARSENAL WANAKARIBIA KUMCHUKUA KIUNGO WA BARCA:



Arsenal wanajiandaa kumnyakuwa kiungo wa Barcelona Sergi Samper na wamejipanga kufikia bei ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20. Arsenal Wenger amemuelezea mchezaji huyo kinda kuwa ndiye mrithi wa Mikel Arteta na yupo tayari kutoa dau la pauni milioni 8.4.

Chanzo: Metro
Jumatano, 7/22/2015 10:23

WEST HAM INAMTAKA CAMBIASSO:



West Ham wapo tayari kumnyakuwa Esteban Cambiasso baada ya kiungo huyo kugoma kuongeza mkataba katika klabu ya Leceister City. The Hammers wanapambana na Barca kukubaliana dili la kumsajili Alex Song na badala yake huenda wakaelekeza mawazo yao kwa mkongwe huyo wa Argentina.

Chanzo: Evening Standard
Jumatano, 7/22/2015 11:36

LIVERPOOL INAMUWINDA DIGNE:



Liverpool imeelekeza sarafu yake kwa mlinzi wa Paris Saint Germain Lucas Digne. Baada ya Christian Benteke kukamilisha usajili wa saba katika klabu hiyo, Brendan Rorgers bado anataka beki wa kushoto, iwe kwa mkopo au kwa dili la kudumu.

Chanzo: Daily Mirror
Jumatano, 7/22/2015 11:32

DILI LA PERISIC KWENDA INTER LIMEKAMILIKA KWA DAU LA EURO MILIONI 18:



Inter Milan na Wolfsburg wamefikia makubaliano kuhusu uhamishao wa Ivan Perisic. Mshambuliaji huyo raia wa Croatia ataigharimu Inter ada ya euro milioni 18.

Chanzo: Corriere dello Sport
Jumatano, 7/22/2015 09:17

PEREZ ANAJIPANGA KUZUNGUMZA NA RAMOS:



Florentino Perez anajipanga kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na Sergio Ramos huko China. Raisi huyo wa Real Madrid atahudhuria Guangzhou na Shanghai kutazama michezo yao ya maandalizi ya msimu na amepanga kujadiliana na beki huyo kuhusu muafaka wake kilabuni hapo.

Chanzo: AS
Jumatano, 7/22/2015 23:49

ASTON VILLA INAMUWANIA ROLAN:



Aston Villa inamuwania Diego Rolan kuchukua nafasi ya Christian Benteke ambaye ametimkia katika klabu ya Liverpool . Newcastle imevutiwa pia, lakini Bordeaux  wanataka euro milioni 20 kwa ajili ya mshambuliaji huyo.

Chanzo: Sud Ouest
Jumatano, 7/22/2015 06:56

0 comments:

Post a Comment