
Mlinda mlango wa klabu ya Arsenal Wojciech Szczesny yupo kwenye harakati za kujiunga na klabu ya Roma kwa mkopo, mtandao wa Goal umetanabaisha.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Poland alipoteza nafasi yake kwa David Ospina mzunguko wa pili wa msimu uliopita wa Ligi Kuu 2014-2015, japokuwa aliichezea Arsenal michezo sita ya FA na kuipatia klabu hiyo kombe hilo mara mbili mfululizo.
Mapema majira haya The Gunners walimsajili Petr Cech kutoka Chelsea kwa ada inayokaribia pauni milioni 11, dili lililosifiwa na wengi kuwa ni wakati wa kilabu hicho kinachonolewa na Arsene Wenger kunyakuwa tena taji kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2004.
Kwa sasa Wenger ameamua kuwa ni Szczesny ndiye atakayeondolewa katika kikosi hicho kuelekea katika kampeni mpya, huku Ospina na Damian martinez wakibakia kutoa upinzani kwa Cech.
Bosi huyo wa The Gunners anaamini kuwa Martinez mwenye umri wa miaka 22, ambaye alisajiliwa kutoka Independiente mwaka 2010, atakuwa tishio katika kilabu hicho hapo baadaye.
Msimu uliopita aliwahi kumjumuisha mlinda mlango huyo wa Kiargentina akidai kuwa kulikuwa na makipa watatu wenye viwango vya dunia "world class" katika vitabu vya Arsenal pale Emirates, msimamo ambao ameutoa walipokuwa wakishiriki Asia Trophy wiki iliyopita.
Imeripotiwa kuwa klabu ya Roma italipa euro 400,000 (pauni 281,000) kwa ajili ya kumchukua kwa mkopo, na watakuwa na fursa ya kufanya dili la kudumu.
Szczesny alikamatwa akivuta sigara kwenye chumba cha kubadilishia nguo kufuatia kipigo kutoka kwa kilabu cha Southampton mwishoni mwa mwaka, huku kukiwa na tetesi za Wenger kukataa kumkacha katika kikosi chake kutokana na matokeo, hakupata tena nafasi kutokea Ligi Kuu mzunguko wote wa pili wa msimu uliopita.
Katika kipindi cha miezi ya mwisho ya kampeni ya 2014-2015 alipokea wito kutoka kwa walinda mlango wa zamani wa Poland Jan Tomaszewski na Jerzy Dudek kujiondoa klabuni hapo, na kabla ya ushindi wa Kombe la FA dhidi ya Aston Villa, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 alilazimishwa na baba yake kujiweka mbali na ukosoaji wa Wenger.
Kwa sasa ataelekea Roma, ambapo Morgan De Sanctis mwenye umri wa miaka 38 alitokea mara 35 kwenye Ligi msimu uliopita.
Giallorossi walimaliza nafasi ya pili katika Serie A msimu uliopita wa mwaka 2014-2015, pointi 17 nyuma ya mabingwa Juventus.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
WOJCIECH SZCZESNY KUJIUNGA NA ROMA KWA MKOPO...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment