ROONEY AREJEA TENA EVERTON TANGU ATIMKIE MAN UTD MWAKA 2004...

Monday, 3 August 2015

In Pictures: Rooney returns to Everton for Ferguson testimonial

Wayne Rooney atinga tena uzi wa Everton kwa mara ya kwanza tangu aihame klabu hiyo mwaka 2004 walipokipiga dhidi ya Villarreal ambapo alishuhudia timu hiyo ikila kichapo cha 2-1 kwenye mchezo wa heshima ya Duncan Ferguson.

Mapokezi ya Rooney yaliambatana na shangwe pamoja na kuzomewa kutoka kwa mashabiki wa nyumbani-wengi wamedhihirisha kuwa hawakufurahishwa na kitendo cha mchezaji huyo kutimka klabuni hapo na kujiunga na Manchester United mnamo mwaka 2004-wakati Ferguson alikaribishwa kwa furaha sana.



Wachezaji hao wawili waliwahi kukipiga pamoja katika kikosi cha kwanza cha kilabu hicho wakati Rooney alipoingia kikosi cha kwanza mwaka 2002, lakini walishindwa kuipa timu hiyo ushindi baada ya Gerard na Matias Nahuel kuipatia Villarreal mabao mawili.

Katika mchezo huo Rooney alikipiga kwa dakika 16 za mwisho na kupokelewa kwa taswira tofauti kutoka kwa mashabiki wa Goodison Park.



0 comments:

Post a Comment