
Timu ya taifa ya Argentina imeanza kwa sare michuano ya Copa America inayoendelea nchini Chile baada ya usiku wa kuamkia leo kutoka 2-2 dhidi ya Paraguay.
Watu wengi walidhani Argentina ingeibuka na ushindi baada ya Sergio Aguero kufunga goli la kuongoza dakika ya 29, kabla ya Lionel Messi kutumbukiza kitu kambani dakika ya 36.
Messi amefunga goli hilo kwa mkwaju wa penalti uliotokana na beki wa Paraguay, Miguel Samudio kumuangusha kwenye eneo la hatari Angel di Maria.
Hadi timu zinakwenda mapumziko, Argentina walikuwa wanaongoza 2-0.
Kipindi cha pili mambo yalibadilika, Paraguay walifunga goli la kwanza dakika ya 60′ kupitia kwa Nelson Valdez na wakasawazisha dakika ya 90 kupitia kwa nyota wa Spartak Moscow, Lucas Barrios.
Mechi nyingine ya kundi B imeshuhudiwa Uruguay ikishinda goli 1-0 dhidi ya Jamaica.
Goli pekee la Uruguay limefungwa dakika ya 52 kupitia kwa Cristian Rodriguez.

Magoli matatu "Hat-Trick" yaliyotupiwa nyavuni dakika ya 28, 65, na 71 na mshambuliaji Andre Schurrle wa timu ya Taifa ya Ujerumani yaliiweka Gibraltar kwenye upanga wa magoli 7-0 katika mashindano ya kuwania kufuzu Euro 2016.
Magoli mengine yaliyoshuhudiwa yaliwekwa kimiani na Max Kruse dakika ya 47 na 81, Ilkay Gundogan dakika ya 51, na Karim Bellarabi dakika 57.
Timu hiyo ya taifa ya Ujerumani iliyokuwa inatumia mfumo wa 3-1-4-2 iliibuka na ushindi wa magoli 7-0 huku kiungo wa Arsenal Mesut Ozil akitoa pasi tatu za magoli hayo.

Mechi nyingine imeshuhudiwa Poland ikiibuka na ushindi wa mabao 4-0 baada ya mshambuliaji wao Robert Lewandowski kutupia magoli matatu "Hat-Trick" ndani ya dakika nne tu.
Robert Lewandowski kwa sasa anaongoza katika safu ya wafungaji akiwa na jumla ya magoli saba na kuisaidia timu yake ya taifa kushikilia usukani wa kundi D.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
ARGENTINA YA MESSI YATOA SARE, UJERUMANI YAUA SABA, LEWANDOWSKI APIGA TATU NDANI YA DAKIKA NNE...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment