MANCHESTER UNITED YAMUWANIA SERGIO RAMOS, ARSENAL KUMKOSA RAHEEM STERLING...

Sunday, 14 June 2015



Klabu ya Manchester United ipo tayari kutumia kitita cha Euro milioni 27.5 kumsajili beki wa Real Madrid Sergio Ramos. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania amekataa kufanya mazungumzo ya mkataba mpya na miamba hao wa La Liga sababu ikiwa ni klabu hiyo kutokukidhi mahitaji yake ya mshahara. Klabu nyingine zinazomuwania mchezaji huyo ni Manchester City na Chelsea.

Baada ya uwezekano wa kumleta mjini Manchester beki wa kati wa Borussia Dortmund Mat Hummels kugonga miamba mara kadhaa, klabu ya Manchester United sasa imeelekeza macho yake kwa mchezaji wa Valencia Nicolas Otamendi na ipo tayari kutoa dau la Euro milioni 50 kumnasa mchezaji huyo.




Arsenal wamekata tamaa ya kumsajili mchezaji wa klabu ya Liverpool Raheem Sterling kutokana na mchezaji huyo kuuzwa bei ghali. Kwa sasa washika bunduki hao wana nia ya kuimarisha kikosi chao katika safu ya kiungo na golini kwa hiyo hawapo tayari kumtumia mchezaji wao Theo Walcott kama sehemu ya mpango wa kumpata Raheem Sterling.



Klabu ya PSG ina mpango wa kutoa upinzani kwa klabu ya Arsenal kwa ajili ya kumuwania golikipa wa klabu ya Chelsea Petr Cech. Klabu hiyo ya Chelsea "The Blues" itamruhusu mlinda  mlango huyo kujiunga na timu pinzani za Uingereza zikiwemo Arsenal na Manchester United.



0 comments:

Post a Comment