
Usain Bolt, mwana riadha mwenye kasi kubwa zaidi duniani, ameonekana kuachia nafasi yake baada ya kukumbwa na majeraha mwaka 2014, wakati mwanariadha mwingine Gatlin akiweka rekodi ya mwaka ya mwanaraidha mwenye kasi na kutangaza kwamba anaweza kumshinda mkongwe huyo.
"Gatlin amekuwa akiongea sana, na kuzungumza mengi" alizungumza Bolt kabla ya mashindano ya adidas Grand Prix katika kisiwa cha Randall.
"Ameweza kudhihirisha kwamba ana kasi na yupo tayari. Kwahiyo itakuwa ni shauku kubwa kuingia katika Mashindano ya Dunia."
"Natarajia zaidi kushindana na majadiliano ya watu...kwa sababu kama hutoyashinda, utaonekana mjinga."

Gatlin, ambaye alifungiwa kushiriki michuano miwili kufuatia shutuma za kutumia madawa ya kuongeza nguvu, mwezi uliopita alikimbia kwa sekunde 9.74-rekodi ya kipekee na ya kasi katika mita 100 mwaka 2015 mjini Doha na kuongoza kwa sekunde 19.68 kwenye michuano ya mita 200 mjini Eugene siku 15 baadae.
Bolt, ambaye anashikilia rekodi ya Dunia katika matukio yote (sekunde 9.58 mita 100 na sekunde 19.19 mita 200), atakimbia mita 200 tu siku ya Jumamosi huku akiendelea kuamsha hisia kwa mashabiki juu ya ushindani utakaoonesha dhidi ya Gatlin.
Hata hivyo Mjamaika huyo amesisitiza uteuzi wake wa mbio hauna uhusiano wowote wa woga dhidi ya wanariadha wengine.
"Hofu?, huwa nacheka nikisikia watu wakisema hivyo, nimekuwa katika mchezo huu kwa miaka sasa, na sijawahi kumkwepa yeyote, inapohitajika siku zote huwa natokea nakuthibitisha mimi ni bora," alisema Bolt.
"Ukweli ni kwamba, sipo katika ubora wangu kwa sasa na sitojitokeza tu kama ninajua ndio nimerudi na nina hitaji muda kufikia pale ninapohitaji."
"Nitakapofika Beijing, nitakuwa tayari na hapo ndipo mmpambano utakuwepo."
Bolt alisema, shauku iliyopo baina ya wakimbiaji wa mbio fupi inaweza leta hamasa kubwa katika Mashindano ya Dunia.
"watu huwa wanakuwa na hamu ya mashindano. Nini kitatokea?," alisema.
"Justin ni mkimbiaji mzuri, Tyson ni mkimbiaji mzuri, Asafa ni mkimbiaji mzuri, Usain ni mkimbiaji mzuri."
"Tutakapofika kwenye mashindano, itakuwa kama mlipuko."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
BOLT: SIMUOGOPI GATLIN....
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment