
Klabu ya Real Madrid inamuwania kiungo wa Monaco Geoffrey Kondogbia.
Klabu hiyo ya Ufaransa inahitaji angalau dau la Euro milioni 35 kumuuza mchezaji huyo.
Klabu ya Arsenal ni miongoni mwa vilabu vikubwa vinavyowania saini ya kiungo huyo.
PSG YAMTAKA PEDRO...

Miamba ya Ufaransa PSG ina nia ya kumsajili winga wa Barcelona Pedro Rodriguez, ingawa winga huyo hivi karibuni alisaini mkataba mpya na miamba hao walionyakua taji la Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya.
Hata hivyo klabu ya PSG bado inaonesha nia ya kuendelea kumshawishi winga huyo ajiunge nao.
REMY APEWA RUHUSA KUONGEA NA WESTHAM...

Mabingwa wa ligi ya Uingereza Chelsea ("The Blues") wamemruhusu mshambuliaji wao Loic Remy kufanya mazungumzo na klabu ya West Ham kuhusiana na usajili.
Mshambuliaji huyo ameonesha nia ya kutaka kutimka klabuni hapo baada ya kocha huyo wa Upton Park kuonesha nia ya kumuhitaji.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MADRID YAMTAKA KONDOGBIA, PSG YAMFUNGIA KAZI PEDRO NA REMY ARUHUSIWA KUZUNGUMZA NA WEST HAM....
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment