
Kiungo wa PSG Yohan Cabaye ametoa tamko kali kwamba atawahama mabingwa hao wa Ligue 1 na kwenda kukipiga katika klabu nyingine msimu ujao.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alijiunga na miamba hiyo akitokea klabu ya Newcastle United mwanzoni mwa mwaka 2014 na kufanikiwa kushinda mataji mawili, medali ya Coupe de la Ligue na Coupe de France wakati wa muda wake mjini Paris.
Lakini kiungo huyo kwa kiasi kikubwa amekuwa mchezaji wa akiba chini ya kocha mkuu Laurent Blanc, na kufanikiwa kuanza mechi 22 za Ligue 1.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 amekuwa akihusishwa kuungana na kocha wake wa zamani wa Newcastle United Alan Pardew ambaye kwa sasa anaifundisha klabu ya Crystal Palace.
"Kuna hali sasa ambapo sikuwa na muda wa kucheza kama nilivyotegemea" aliiambia Infosport+.
"Wawakilishi wangu wanatafuta ufumbuzi sahihi. Katika siku zijazo, jambo muhimu ni kucheza kila mwisho wa wiki."
Alipoulizwa kuhusu kurudi Ligi Kuu ya Uingereza, Cabaye aliongeza: [Ni] Ligi ninayoipenda, nchi pia.
"Kunaweza kuwa na nafasi, kama kunaweza kuwa na watu wengine. Jambo muhimu ni kwamba nitafikiria kwa makini na kufanya maamuzi sahihi."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
CABAYE: "NATAKA KUCHEZA KILA WIKI..."
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment