
Licha ya kutupwa nje ya michuano ya Copa America na timu ya Paraguay, wachezaji wa kikosi cha Brazil walipokelewa kwa shangwe na mashaiki wa nchi hiyo waliojitokeza kwa wingi uwanja wa ndege kuwalaki wachezaji wao waliokuwa wanarudi kutoka nchini Chilile ambako walitupwa nje ya mashindano hayo kwachangamoto ya mikwaju ya penati na timu ya Paraguay.

Tofauti na ilivyokuwa inanatarajiwa na watu wengi, baada ya kutupwa nje kwenye hatua ya robo fainali ya michuano hiyo mikubwa kwenye bara la Amerika ya Kusini, lakini bado mashabiki walijitokeza kwa wingi kuwapokea wachezaji wao na kupiga nao picha ‘selfies’ mara baada ya kutua kwenye ardhi ya kwao.

Robinho, David Luiz, Willian na Dunga wote kwa pamoja ‘wali-post’ kwenye account zao za mitandao ya kijamii picha mbalimbali walizopiga wakiwa na mashabiki mara baada ya kutua jijini Sao Paulo, Brazil.




Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
CHEKI PICHA ZA MAPOKEZI YA BRAZIL BAADA YA KUTUPWA NJE YA COPA AMERICA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment