
Wakati Liverpool wakikataa ofa ya pauni milioni 25 kutoka Manchester City kumsajili Raheem Sterling, Chelsea na Liverpool wanamgombea Radamel Falcao.
Liverpool wamesema kwamba hawana nia ya kumuuza mchezaji huyo, lakini Man City wanatarajia kurejea na ofa kubwa zaidi.
Sterling, 20, amekataa mkataba mpya wa pauni 100,000 kwa wiki Anfield, akisema anataka kucheza klabu kubwa inayotwaa makombe, ambapo anahusishwa pia na Arsenal na tayari ameuza nyumba yake Liverpool akitafuta nyingine London.
Bosi mpya wa Real Madrid aliyepata kuwafundisha Liverpool, Rafa Benitez amesema anapenda mchezaji wa aina ya Sterling lakini kocha wa Liver, Brendan Rodgers amesema anaamini mchezaji wake huyo atabaki Anfield msimu ujao.

Pamoja na mambo mengine, City wanajitahidi kupata mchezaji Mwingereza ili kulandana na kanuni za soka, kwani baada ya kuondoka kwa James Milner, Frank Lampard na Micah Richards, Mwingereza pekee aliyebaki ni kipa Joe Hart.
Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho amesema anataka kumsaidia mshambuliaji wa kati wa Colombia, Radamel Falcao kurejea kwenye kiwango cha juu.
Mourinho ameahidi kufanya hivyo, akieleza kusikitishwa kwake na watu wanaomchagiza na kudhani kwamba Falcao wa kweli ni aliyeonekana Man United msimu ulionalizika.
Chelsea wamekuwa kwenye mazungumzo kumpata mpachika mabao huyo aliyeshindwa kuwika msimu uliopita lakini kinachogomba ni mshahara wake wa pauni 265,000 kwa wiki.
Liverpool wanamhitaji Falcao, 29, ili kunoa safu ya ushambuliaji ambayo imekuwa doro tangu kuondoka kwa Luis Suarez aliyekwenda Barcelona na kuumia mara kwa mara kwa ‘pacha’ wake wa msimu juzi, Daniel Sturridge.
Kadhalika huenda wakamhitaji iwapo Sterling ataondoka au kushindwa kucheza kwa kiwango, kwani tayari ameanza kuzomewa na washabiki wa Liver. Mshambuliaji mwingine ni Mario Balotelli aliyefunga bao moja msimu mzima.
Manchester United wanasema wapo tayari kutoa ofa kwa ajili ya kumnasa mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane, 21.
United tayari wamekubaliana na klabu ya Hoffenheim juu ya ada ya pauni milioni 13 kwa ajili ya kumpeleka Old Trafford mshambuliaji Roberto Firmino, 23.

Mshambuliaji Jackson Martinez, 28, anayewaniwa na Arsenal na Manchester United anasema kwamba ana nia ya kuondoka Porto na kujiunga na klabu kubwa zaidi ya Ulaya.
Real Madrid wamedhamiria kukubaliana na Man U ili kumsajili kipa wao, David De Gea, 24, kabla ya safari yao ya Australia Julai 13. Inaelezwa kwamba De Gea akishaanza kuwaaga wachezaji wenzake wa United.
West Ham wapo kwenye mazungumzo ya kumsajili moja kwa moja kiungo wa Barcelona, Alex Song, 27, waliyekuwa naye kwa mkopo msimu uliopita ikielezwa ada ni kwenye pauni milioni tano.
Kadhalika wanataka kumsajili winga wa Marseille, Dimitri Payet, 28. Kocha wao mpya, Slaven Bilic aliyekuwa mlinzi wa klabu hiyo anasema kurejea hapo ni kama kulamba bingo mara mbili.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
DAU LA MAN CITY LAKATALIWA, FALCAO NDANI, CECH NJE CHELSEA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment