
Kiungo wa klabu ya Arsenal Aaron Ramsey amechagua wachezaji kutoka nyumbani na nje ya nyumbani-uchaguzi wa kushangaza na uteuzi wa wachezaji nyota wa timu pinzani-kutengeneza mchezaji wa teknolojia ya kibayoniki (Bionic Footballer).
Nani ni mchezaji mzuri kwa sasa? Tumeshalizungumza sana. Lionel Messi na Cristiano Ronaldo ndio bora zaidi kwa sasa-labda kama wewe ni shabiki namba moja wa Javier Mascherano kama Roy Hodgson.
Lakini itakuwaje kama utachanganya na kufananisha? vipi kama Andrea Pirlo angekuwa na guu la kushoto la Messi au Ronaldo angekuwa na muono wa Xavi?
Hivi karibuni tovuti ya Goal imezungumza na Aaron Ramsey kuhusiana na swala hilo. Kiuhalisia alijichagua mwenyewe kama sehemu ya mchezaji wake huyo wa kipekee. Lakini ni nani mwingine alitengeneza daraja? Spoiler: Ronaldo sio mmoja wapo.
Kulikuwa na mishangao michache kwa mchezaji huyo wa Arsenal akitoa heshima kwa chimbuko lake, na pia kwa mashujaa wa Chelsea na wachapakazi wa Liverpool wakihusishwa.
Baada ya kumaliza uchunguzi wa Kibayomekaniki (Biomechanical Tests) kwa ajili ya uwiano mpya, Ramsey alimchagua mchezaji wake huyo wa kibayoniki (Bionic Footballer).
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MESSI, BALE, CAZORLA....AARON RAMSEY AMTENGENEZA MCHEZAJI WA AINA YAKE...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment