MONACO-Ruben Loftus-Cheek, Nathan Ake and Andreas Christensen:

Klabu ya Monaco imepanga kuwachukuwa kwa mkopo wachezaji watatu kutoka katika klabu ya Chelsea ikiwa kama ni moja ya mipango ya klabu hiyo kuwapatia kwa mkopo mshambuliaji Radamel Falcao. Wachezaji hao ni pamoja na Ruben Loftus-Cheek, Nathan Ake na Andreas Christensen.
ATLETICO MADRID-MARTINEZ:

Mchezaji wa kimataifa wa Colombia Jackson Martinez mwenye umri wa miaka 28 amethibitisha kuwa atajiunga na klabu ya Atletico Madrid kutoka klabu ya Porto kwa ada ya pauni milioni 24.8 na atapatiwa mkataba wa miaka minne.
LIVERPOOL-LLORENTE:

Baada ya Juventus kumpata mshambuliaji Mario Mandzukic kutoka Atletico Madrid, mshambuliaji aliyekuwa klabuni hapo Fernando Llorente anatazamiwa kujiunga na klabu ya Liverpool. Liverpool imekuwa ikimuhitaji mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30.
ARSENAL-EZEQUIEL GARAY:

Klabu ya Arsenal inaongoza mbio za kumuwania mlinzi wa kati wa klabu ya Zenit Ezequiel Garay. Klabu hiyo ya Uingereza imetoa ofa ya pauni milioni 13 ili kumnasa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. Klabu ya Manchester United ilihusishwa pia na mchezaji huyo.
TOTTENHAM-VICTOR MOSES:

Baada ya kuwa na kizungumkuti katika klabu ya Chelsea, Tottenham imepanga kufanya usajili wa kushitukiza wa mchezaji wa klabu hiyo Victor Moses. Mchezaji huyo amekuwa akihusishwa na kujiunga moja kwa moja na klabu ya Stoke City ambapo alikipiga kwa mkopo msimu uliokwisha, lakini huenda mpango huo akauchelewesha baada ya Spurs kuonesha nia.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
FALCAO KUBADILISHWA NA WACHEZAJI WATATU CHELSEA, GARAY KUTUA ARSENAL, LLORENTE AJIPELEKA LIVERPOOL...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment