MANCHESTER CITY-WILSHERE:

Manchester City inajiandaa kutoa dau la pauni milioni 40 ili kumpata kiungo wa klabu ya Arsenal Jack Wilshere kama watamkosa kiungo wa miamba ya Italia klabu ya Juventus Paul Pogba. Manchester City wapo tayari kumlipa kiungo huyo mshahara wa pauni 150,000 kwa wiki.
MANCHESTER UTD-OTAMENDI:

Mlinzi wa klabu ya Valencia Nicolas Otamendi amewaambia marafiki zake kuwa yupo tayari kujiunga na klabu ya Manchester Utd. Valencia imewataka Manchester United kulipa dau la pauni milioni 35 kumnasa mchezaji huyo.
CHELSEA-ALDERWEIRELD:

Meneja wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho anachelewesha mpango wa kubadilishana wachezaji kati ya Filipe Luis na Toby Alderweireld huku akiangalia namna nyingine ya kupata mlinzi mpya katika klabu hiyo.
PSG-GRIEZMANN:

PSG imetoa ofa yake ya euro milioni 40 kwa klabu ya Atletico Madrid kwa ajili ya kupata saini ya mchezaji Antoine Griezmann. Mabingwa hao wa Ufaransa wameachana na mawazo ya kumpata mchezaji wa Manchester United Angel Di Maria na mchezaji wa Juventus Paul Pogba.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MAN CITY YATENGA £40 MILIONI KUMPATA WILSHERE, OTAMENDI ATOA TAMKO KUHUSU MAN UTD...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment