REAL MADRID-SERGIO RAMOS

Taarifa kutoka Hispania zinaeleza kuwa mazungumzo kati ya Real Madrid na beki wake wa kati Sergio Ramos yamevunjika, huku wakala wa mchezaji huyo akizungumza na mmoja wa wagombea uraisi wa klabu ya Barcelona Jordi Majo kuhusiana na mchezaji huyo kutua katika klabu hiyo.
MANCHESTER UTD-FIRMINO

Mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino amekubali ofa kutoka Manchester United, hili ni pigo kwa klabu pinzani ya Liverpool ambayo ilikuwa ikimuwania mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazili. Nyota huyo atatua katika klabu ya Manchester United kwa dau la euro milioni 21.
ARSENAL-SVEN BENDER & SOKRATIS PAPASTATHOPOULOS

Arsene Wenger anafikiria kutoa ofa kwa wachezaji wawili wa klabu ya Borussia Dortmund Sven Bender na Sokratis Papastathopoulos. Bosi mpya wa Thomas Tuchel yupo tayari kuwauza wachezaji hao ili kusuka kikosi chake na klabu ya Arsenal ipo tayari kutoa ada ya euro milioni 42 kwa wachezaji hao.
LIVERPOOL-MATEO KOVACIC

Baada ya Steven Gerrard kuondoka, kocha wa Liverpool Brendan Rodgers ana nia ya kumleta kiungo mpya katika klabu hiyo na anamtaka nyota wa Inter Mateo Kovacic. Wekundu hao wako tayari kutoa dau la euro milioni 30.
ARSENAL-PETR CECH

Arsenal ipo tayari kumfanya Petr Cech kuwa golikipa anayelipwa pesa nyingi katika klabu hiyo na mmoja ya wachezaji watakao kuwa wanapokea mshahara zaidi ya £ 100,000 kwa wiki katika klabu hiyo. Mchazaji huyo wa kimataifa wa Czech anajianda kuondoka Chelsea, lakini Arsenal wanaweza kupata upinzani kutoka PSG ambayo inamuwania kipa huyo.
ARSENAL-ARTURO VIDAL

Manchester United na Real Madrid wamejitoa kwenye mbio za kumuwania kiungo wa Juventus Arturo Vidal baada ya kukamatwa akiendesha gari huku amelewa. Hii inaiachia njia klabu ya Arsenal kumsajili kiungo huyo.
BARCELONA-PAUL POGBA

Ripoti kutoka Barcelona zinadai kuwa klabu hiyo ipo tayari kuwauza baadhi ya wachezaji ili kujipatia kiasi cha pesa cha euro milioni 100 ili kumnunua kiungo wa klabu ya Juventus Paul Pogba.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
RAMOS AITAMANI BARCELONA, CECH KULIPWA MSHAHARA MNONO ARSENAL...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment