MANCHESTER UTD YAMUWANIA FABINHO, OTAMENDI; CHELSEA INAMTAKA OXLADE CHAMBERLAIN...

Wednesday, 17 June 2015

MANCHESTER UTD-FABINHO, OTAMENDI:



Klabu ya Manchester United imesema ina nia ya kumsajili beki wa pembeni wa Monaco Fabinho na wana mpango wa kutoa dau la pauni milioni 10 ili kupata saini ya beki huyo. Mabingwa wa Ligi ya Mabingwa  Barani Ulaya klabu ya Barcelona nayo imeonesha nia ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 mwenye mkataba na Monaco mpaka mwaka 2019.



Wakati huo huo klabu hiyo ya Manchester United itamenyana vikali na klabu ya Real Madrid katika vita ya kupata saini ya mchezaji wa kimataifa wa Argentina Nicolas Otamendi. Rafael Benitez amekiri kuvutia na mchezaji huyo na kufanya mazungumzo na wakala wa mchezaji huyo ili kufanikisha dili hilo.


MAN CITY-STERLING



Klabu ya Liverpool imekataa tena dau la pauni milioni 40 lililotolewa na klabu ya Manchester City kwa ajili ya kumpata winga wa klabu hiyo Raheem Sterling. Klabu hiyo ya Liverpool inasema mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza anauzwa pauni milioni 50.


CHELSEA-BEGOVIC:



Klabu ya Chelsea imeonesha nia ya kumsajili golikipa Asmir Begovic kama mbadala wa kudumu wa kipa Petr Cech ambaye ameomba kutimka klabuni hapo lakini huenda dili hilo likaingia shubiri baada ya kipa huyo kusema hawezi kuwa kipa namba mbili nyuma ya kipa wa sasa Thibaut Courtois.

CHELSEA-ALEX OXLADE CHAMBERLAIN:


Klabu ya Chelsea inajiandaa kutoa dau la pauni milioni 20 kwa ajili ya kumchukua mchezaji wa klabu ya Arsenal Alex Oxlade -Chamberlain. The Blues hawapo tayari kumtumia kipa wao Petr Cech kama sehemu ya mpango huo.

0 comments:

Post a Comment