
Thierry Henry anahisi Jackson Martinez atang'aa katika klabu ya Arsenal huku kukiwa na uvumi kuwa mchezaji huyo atatua katika uwanja wa Emirates.
Wiki iliyopita iliaminika kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 yupo mbioni kujiunga na klabu ya AC Milan kutoka Porto, ingawa mchezaji huyo amekanusha habari hizo.
Mwezi wa pili meneja wa Arsenal Arsene Wenger alizungumzia kuhusu mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Colombia, akisisitiza mshambuliaji "yupo katika orodha ya vilabu vingi," na shujaa wa klabu hiyo Henry amemsifia Martinez kufuatia uamuzi wake unaotarajiwa.
"Jackson Martinez anaweza kufiti vizuri." Henry aliwaambia waandishi wa habari. "Lakini tayari unaye Giroud ambaye kiasi wanafanana kama mshambuliaji."

"Anaweza kuwa nyongeza nzuri katika kikosi. Alikuwa na msimu mzuri katika Ligi ya Mabingwa, lakini tayari una watu."
"Nadhani Giroud ni zaidi au chini ya mchezaji wa aina hiyo. Nadhani Martinez ana nguvu kiasi na anaweza kurudi nyuma kusaidia lakini tutaona ni nini Arsene Wenger atafanya."
"Kwa ujumla, washambuliaji wa Arsenal hawakufanya vibaya msimu uliokwisha."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
"MARTINEZ ATANG'AA AKITUA ARSENAL"-THIERRY HENRY
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment