
Nahodha wa timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi alikataa tuzo ya mchezaji wa mechi baada ya timu yake kutoa sare ya 2-2 dhidi ya timu ya taifa ya Paraguay, kwasababu alikuwa na hasira baada ya kupoteza pointi mbili katika mechi hiyo ya ufunguzi ya mashindano ya Copa Amerika.
Messi ambaye aliisaidia timu yake kupata goli la pili kupitia mkwaju wa penati baada ya Kun Aguero kuipatia timu hiyo bao la kuongoza hakuwa na hamu ya picha baada ya filimbi ya mwisho kupulizwa siku ya Jumamosi.
Mwakilishi kutoka MasterCard, ambaye huwa anatoa tuzo hizo kwenye mashindano ya bara, alikwenda kwenye chumba cha Argentina cha kubadilishia nguo kumjulisha mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kuwa amechaguliwa kama mchezaji wa mechi lakini aliambiwa kuwa Messi hawezi kupokea tuzo hiyo.
Kufuatia kukataa kwa mshambuliaji huyo wa Barcelona, MasterCard walikuwa na nia ya kumchagua mchezaji mwingine kutoka kwenye kikosi cha vijana hao wa Gerardo Martino lakini hakuna mchezaji aliyekuwa tayari kupokea tuzo hiyo.
Baadae tuzo hiyo ilipendekezwa itolewe kwa mmoja wa wachezaji waliofunga mabao kutoka timu pinzani, kati ya Nelson Valdez ambaye aliipatia timu yake goli la kuongoza au Lucas Barrios ambaye aliipatia timu yake bao la kusawazisha.
Leo katika mchezo wa kundi B Argentina watamenyana vikali na timu ya Uruguay.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MESSI AIKATAA TUZO YA MCHEZAJI WA MECHI...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment