
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mambo ya umma wa Shirikisho La Mpira Duniani (FIFA) ameamua kuachia ngazi hiyo.
Walter De Gregorio alifanya kazi katika chombo cha kusimamia michezo tangu Septemba 14, mwaka 2011 na ataendelea kuwa mshauri wa Shirikisho hilo hadi mwishoni mwa mwaka huu.
Hata hivyo, naibu wake, Nicolas Maingot, amekaimu nafasi hiyo kwa muda.
"Walter amefanya kazi kwa bidii na kwa kujitoa kwa miaka minne na tunashukuru kwa dhati kwa yote aliyoyafanya," Katibu Mkuu Jerome Valcke aliiambia rasmi tovuti ya shirika hilo.
"Nafurahi bado tutaendelea kufanya kazi chini ya utaalamu wake hadi mwishoni mwa mwaka huu"
Uswisi-Italia inasadikiwa kuwa moja kati ya msaada mkubwa kwa Raisi wa Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA) Sepp Blatter, ambaye wiki iliyopita alitangaza kujiuzulu kutokana na kuibuka kwa sakata la rushwa ambalo limekumba shirikisho hilo.
De Gregorio alisimamia mikutano ya wanahabari ambayo ilihusisha kujiuzulu kwa Raisi wa Shirikisho hilo Sepp Blatter pamoja na kutoa uthibitisho kwamba kuna maofisa wa FIFA walikamatwa, zoezi lililoendeshwa na Shirika la KIjasusi la Marekani (FBI) kuhusiana na shutuma za hongo tangu mwaka 1991.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MKURUGENZI WA MAWASILIANO NA MAMBO YA UMMA WA FIFA AACHIA NGAZI
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment