
Meneja Wa Chelsea Jose Mourinho amesema kwamba usajili wake wa kwanza anaoupa kipaumbele ni kuwalinda wachezaji bora waliopo wasiondoke klabuni hapo, lakini ameahidi kuongeza watatu katika kikosi kilichotwaa ubingwa msimu uliokwisha.
Baada ya Chelsea "The Blues" kufanikiwa kushinda taji la ligi msimu wa 2014-2015, mreno huyo ana nia ya kudumisha mawazo ya kushinda bila kufanya mabadiliko ya kutosha katika kikosi chake kilichotwaa taji hilo.
Ingawa kocha huyo anatafuta mchezaji wa kuziba nafasi ya mshambuliaji Didier Drogba ikiwa pamoja na kuongeza wachezaji wachache ili kuongeza ushindani wa ziada katika safu yake, Mourinho anatarajia kupambana na vilabu pinzani vitakavyojaribu kununua nyota wake.
"Misimu mingine, nilikuwa na furaha sana kuuza baadhi ya wachezaji, hata waliokuwa wazuri-lakini mwaka huu sina raha kuuza wachezaji wangu bora, kwa hiyo changamoto niliyonayo ni kuwafanya wabaki hapa," mreno huyo alinukuliwa na Mirror.
"Nikiwabakiza [Eden] HAzard, [Nemanja] Matic, [Branislav] Ivanovic, [Diego] Costa na [Cesc] Fabregas, hilo ni lengo kuu la kwanza."
"Nadhani tunahitaji wachezaji watatu-mshambuliaji, kwa sababu tumempoteza shujaa wetu [Drogba], beki na kiungo ili kuongeza ushindani zaidi, kuongeza damu mpya katika kikosi inaleta ushindani kwa wachezaji waliopo."
"Wanahitaji kutambua kuwa kuna mtu anasubiri nafasi zao-wao ni mabingwa sasa, ninahitaji hilo kudumisha namna ya ufanyaji wangu kazi. Lakini kimsingi, ninahitaji kuweka wachezaji wale wale, kikosi kile kile, meneja yule yule, na kuleta utulivu katika klabu."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MOURINHO KUONGEZA WATATU CHELSEA
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment