
Kiungo wa kimataifa wa Brazili na klabu ya Hoffenheim Roberto Firmino atajiunga na klabu mojawapo ya Ligi Kuu Uingereza, kwa mujibu wa wakala wake.
Imeripotiwa kuwa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 ameivutia klabu ya Manchester United baada ya kufanya vizuri huko Bundesliga, amefunga magoli 49 katika mechi 153, na ushindi alioipatia Brazili dhidi ya Honduras kwenye mashindano ya Copa Amerika umempa nafasi kubwa ya kutua Ligi Kuu Uingereza.
Firmino alisaini mkataba mpya wa miaka mitatu katika klabu yake ya Hoffenheim mwaka 2014 , lakini Louis van Gaal anasadikika kuwa karibu kukubaliana na mpango wa kumsajili kwa ada ya pauni milioni 13.
"Ninachoweza kusema ni kwamba atakwenda Uingereza, " Roger Wittmann alinukuliwa akizungumza na Bild.
Liverpool pia wamekuwa wakihusishwa kuwania saini ya Firmino baada ya Raheem Sterling kusema ataondoka Anfield kutafuta malisho mapya.

Hivi karibuni Firmino aliingia kama mchezaji wa akiba akitokea benchi kama mbadala wa Fred katika mechi dhidi ya Peru ambapo Brazil iliibuka na ushindi wa goli 2-1 kwenye mashindano ya Copa Amerika Jumapili jioni.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
ROBERTO FIRMINO KUCHEZA MANCHESTER UTD MSIMU UJAO...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment