
Kocha wa Galatasaray Hamza Hamzaoglu ametanabaisha kuwa klabu yake ina nia ya kumleta Uturuki mshambuliaji wa Manchester United Robin van Persie.
Muelekeo wa mchezaji huyo klabuni hapo haujafahamika, huku kocha wa klabu hiyo Louis van Gaal akifikiria kumuondoa mholanzi mwenzake katika klabu hiyo ili kuacha nafasi kwa mshambuliaji mpya.
Mabingwa wa Italia Juventus na klabu ya Serie A Lazio zote zimehusishwa katika mbio za kumuwania mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu ya Arsenal, ambaye alifunga magoli 10 kati ya mechi 27 za Ligi Kuu msimu uliopita.
Galatasaray inaonekana kuwa mbele katika mbio hizo, na Hamzaoglu-ambaye aliiongoza klabu hiyo kunyakuwa ubingwa wa Uturuki msimu wa 2014-2015-kuwa na nia ya kumleta mshambuliaji huyo katika kikosi chake.
"Tunataka kusajili wachezaji ambao wataimarisha kikosi chetu na pia watawafurahisha mashabiki," aliiambia Fanatik.
"Hakuna meneja anayeweza kusema 'Hapana' kwa Van Persie. Hata hivyo hatuwezi kutumia kuzidi kiwango chetu. Tuna matumaini sisi na yeye tutafikia muafaka."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
ROBIN VAN PERSIE KUTIMKIA ZAKE UTURUKI...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment