AXEL WITSEL NA BABA RAHMAN NDANI, MIKEL OBI NJE CHELSEA...

Thursday, 18 June 2015

Mourinho targets Witsel as Chelsea put Mikel up for sale

Chelsea inamnyemelea kiungo wa Zenit St Petersburg Axel Witsel ambapo kocha wa klabu hiyo Jose Mourinho amepanga kukiimarisha kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao.

The Blues imemuelezea Witsel kuonesha kumuhitaji huku klabu hiyo ikionesha nia ya kutaka kujiimarisha katika kiungo, wakati John Obi Mikel akipanga kutimka klabuni hapo kujiunga na klabu za Uturuki au Mashariki ya Kati.

Witsel, mwenye umri wa miaka 26, anampango wa kutimka katika klabu yake ya sasa Zenit St Petersburg msimu huu na ana nia ya kujiunga na miamba wa Italia klabu ya Juventus, lakini chelsea wanaamini mchezaji huyo atajiunga na klabu yao.



Witsel anaaminika kuwa atakuwa mbadala wa kudumu wa Mikel Obi ambaye anaweza kutimka klabuni hapo baadaya ya kuambia yupo huru kuondoka.

Chelsea wanaimani kubwa ya kumchukua mchezaji huyo kwakuwa anatumia wakala mmoja na kocha wa klabu hiyo Jose Mourinho.

Zenit walitumia dau la euro milioni 40 kupata saini ya kiungo huyo kutoka klabu ya Benfica mwaka 2012 lakini amesema anataka kujiunga na klabu nyingine baada ya kunyakua taji na mabingwa hao.

Kwa sasa, Chelsea wanafikiria kumsajili beki wa kushoto wa klabu ya Augsburg Baba Rahman. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ghana mwenye umri wa miaka 20 amehusishwa na kujiunga na klabu ya Chelsea baada ya kufanya vema Bundesliga.

0 comments:

Post a Comment