Kocha mkuu wa timu ya Queretaro ya nchini Mexico imebainisha mipango yake ya kuachana na mwanasoka nguli wa Brazil Ronaldinho Gaucho kwa kushindwa kucheza katika kiwango chake cha juu kama ilivyokua awali.

Kushuka kwa kiwango cha mwanandinga huyo kimechagiwa na umri wake kuwa mkubwa. Mchezaji huyo kwa sasa ana umri wa miaka 34 hivyo kushindwa kufikia makali yake tangu alipojiunga na miamba hiyo ya Mexico.
"Inategemea na sababu mbalimbali, lakini swala ni kwamba yeye [Ronadinho] hatoshiriki tena kwa ajili yetu," Vucetich aliwaambia waandishi wa habari Jumanne.
Akiendelea kubainisha hayo kocha huyo ametanabaisha kuwa nje ya uwanja kimasoko, mchezaji huyo amekua sehemu kubwa ya mafanikio ya klabu hiyo lakini kwa sasa timu yake inataka wachezaji wenye nguvu ya kuisaidia timu katika nyanja zote, nje na ndani ya uwanja.
Ronaldinho amefunga mabao nane kunako klabuni hapo tangu alipowasili akitokea Athletico Mineiro ya Brazil mwaka 2014.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
RONALDINHO KUTUPIWA VIRAGO MEXICO
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment