
Juventus imethibitisha kuwa itamsajili kiungo wa Real Madrid Sami Khedira baada ya mkataba wake na klabu hiyo kuisha baadae mwezi huu.
Msimu uliopita mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Ujerumani alikataa kuongeza mkataba wa kuendelea kuichezea klabu hiyo msimu ujao.
Khedira amekuwa akihusishwa na kurejea tena Bundesliga kujiunga na Schalke 04 huku timu za Uingereza kama Chelsea na Arsenal zikionesha nia ya kumtaka kiungo huyo lakini mshindi huyo wa kombe la dunia amechagua kuelekea mjini Turin.
"Klabu ya Juventus imepata saini ya Sami Khedira leo," taarifa iliyotolewa rasmi na tovuti ya Bianconeri siku ya Jumanne.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28 atajiunga na miamba hao wa Italia kutoka Real Madrid kama mchezaji huru tarehe 1/7/2015. Sami Khedira amekubaliana na miamba hao mkataba utakao muweka klabuni hapo mpaka tarehe 30/6/2019.
Bianconeri bosi, Massimiliano Allegri ana mpango wakuongeza wachezaji wenye viwango vya juu na wenye uzoefu wa kimataifa katika klabu hiyo.
Khedira atahitaji kupambana ili kuweza kupata namba katika kikosi cha kwanza mbele ya viungo wengine kama Claudio Marchisio, Arturo Vidal, Andrea Pirlo na Paul Pogba.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
SAMI KHEDIRA ATIMKIA JUVENTUS...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment