ARSENAL-ARTURO VIDAL:

Klabu ya Arsenal inajiandaa kutoa dau la pauni milioni 21 kumpata kiungo wa Juventus Arturo Vidal. Mchezaji huyo wa Chile ana nia ya kuungana na mchezaji mwenzake wa taifa Alexis Sanchez ambaye alitua klabuni hapo msimu uliopita akitokea Barcelona..
MANCHESTER UTD- SERGIO RAMOS:

Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.

Manchester United wapo mbioni kukamilisha usajili wa kiungo Morgan Schneiderlin wiki ijayo. Mfaransa huyo anataraji kusaini mkataba wa miaka minne klabuni hapo.

Manchester United imepanga kukataa ofa itakayotolewa na klabu ya Ujerumani Bayern Munich kwa ajili ya kumsajili winga Angel Di Maria. Kocha wa Bayern Munich Pep Guardiola anatamani kumsajili winga huyo huku mashetani hao wakiwa hawana nia ya kumuuza mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina.
REAL MADRID-NICOLAS OTAMENDI:

Real Madrid wanajiandaa kuhamia kwa Nicolas Otamendi kama mbadala wa beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos anayehusishwa na kutimka klabuni hapo kuelekea Manchester United.
MAN CITY-PAUL POGBA:

Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
SANCHEZ KUMLETA ARTURO ARSENAL, SCHNEIDERLIN KUSAINI MIAKA 4 MAN UTD, MADRID WAKATAA DAU LA MAN UTD, POGBA KUTUA MAN CITY KABLA YA STERLING...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment