ARSENAL - PEDRO

Arsenal wamefanya mazungumzo na mwakilishi wa mshambuliaji wa klabu ya Barcelona Pedro kuhusu uwezekano wa kumsajili mchezaji huyo msimu huu.
Chanzo: Independent
Jumatatu, Julai 6, 2015 00:29
AC MILAN - IBRAHIMOVIC

Licha ya kuwasajili Carlos Bacca na Luiz Adriano, Milan bado wanamatumaini ya kumnasa Ibrahimovic. Hata hivyo Rossoneri itamlazimu afanye jitihada za juu na kutoa ofa ya kutosha ili waweze kumnasa mchezaji huyo.
Chanzo: Corriere dello Sport
Jumatatu, Julai 6, 2015 07:40
MANCHESTER UNITED - FERNANDO MUSLERA

Manchester United imetenga kiasi cha euro milioni 35 kwa ajili ya golikipa wa Galatasaray Fernando Muslera. Golikipa huyo wa Uruguay amekuwa akitambuliwa kama mrithi wa David de Gea.
Chanzo: Vatan
Jumatatu, Julai 6, 2015 00:26
TOTTENHAM - YANNICK FERREIRA

Tottenham wameripotiwa kutenga kiasi cha £18 milioni kwa ajili Yannick Ferreira Carrasco. Timu hiyo ya Londoni ya kaskazini ilipeleka euro milioni 14 ambazo zilikataliwa na Monaco kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21.
Chanzo: Daily Star
Jumatatu, Julai 6, 2015 00:31
ROMA - JUAN CUADRADO

Klabu ya Roma imerejea kwenye kinyang'anyiro cha kumnasa winga wa Chelsea Juan Cuadrado.
Chanzo: Tuttosport
Jumatatu, Julai 6, 2015 07:16
PSG & MONACO - HACHIM MASTOUR

Paris Saint-Germain na Monaco zote zimeonesha nia ya kumsajili kiungo wa Ac Milan mwenye miaka 17 Hachim Mastour.
Chanzo: L'Equipe
Jumatatu, Julai 6, 2015 07:31
FIORENTINA, GATASARAY & NAPOLI - RAFFAEL

Fiorentina , Galatasaray na Napoli wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumuwania beki wa kulia wa Manchester United Rafael. Mchezaji huyo wa kimataiffa wa Brazili anachukuliwa kama mchezaji wa akiba pale Old Trafford na anatazamiwa kuondoka klabuni hapo, pia klabu mbili za Ligi Kuu zinamhitaji.
Chanzo: Daily Mail
Jumatatu, Julai 6, 2015 16:57
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
ARSENAL YAONGEA NA WAKALA WA PEDRO,AC MILAN YARUDI KWA IBRAHIMOVIC,TOTTENHAM YAMSAKA YANNICK...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment