FENERBAHCE - LUIS NANI

Klabu ya Fenerbahce imetangaza kumsajili Nani kutoka Manchester United.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa ureno aliwasili nchini Uturuki siku ya Jumapili kwa ajili ya vipimo vya afya ili kukamilisha dili la kumnyakua mchezaji huyo baada ya klabu ya Super Lig kukubaliana na Red Devils.

Na klabu hiyo imethibitisha kuwa winga huyo mwenye miaka 28 atakuwa mchezaji rasmi wa Fenerbahce siku ya jumatatu saa 17:00 jioni katika uwanja wa Sukru Saracoglu, ambapo watawaalika mashabiki na waandishi wa habari kuhudhuria hafla hiyo.
Nani alizungumza kwa furaha huku akiwa na shauku ya kucheza katika jiji la Istanbul baada ya kupokelewa na mashsbiki wengi uwanja wa ndege.

"Kwa kweli ninafuraha kuwa hapa," alisema.
"Mimi naona hii ni kama fursa mpya katika kazi yangu. Pia ni fursa ya kujionesha mwenyewe. Pia nahitaji kuwa na mafanikio.
"Niliwaona mashabaki wakija kunitazama na nilikuwa na furaha sana. Nataka niwaoneshe mpira wangu wa ukweli.Daima huwa nafanya kile kilicho bora pale ninapoweza.
"Fenerbahce ni klabu niliyokuwa naifaham. Fenerbahce ni klabu yenye malengo ya kuwa klabu kubwa."

Nani, aliecheza Old Trafford kwa miaka nane,alikuwa kwa mkopo katika klabu ya Sporting Lisbon msimu wa 2014-15, na kucheza mechi 27 za Primeira Liga.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
LUIS NANI ATUA FENERBAHCE RASMI...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment