
Baada ya mshambuliaji chipukizi wa kilabu cha vijana cha Arsenal Chuba Akpom kutupia magoli matatu katika mchezo dhidi ya mastaa wa Singapore, kocha wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger amesema anataka kumuweka mshambuliaji huyo kwenye kikosi cha kwanza msimu huu na hatomtoa tena kwa mkopo.
Akpom amefanikiwa kutokea kwenye kikosi cha wakubwa mara nne tu tangu alipojiunga na timu ya watoto akiwa na miaka 6, lakini mwezi wa pili aliongeza mkataba wa muda mrefu na klabu hiyo.
Amevichezea kwa mkopo vilabu kadhaa zikiwemo timu za Brentford, Coventry City and Nottingham Forest ndani ya miaka miwili iliyopita ambapo alishindwa kuonesha makali yake, lakini Arsene Wenger amesisitiza kuwa mshambuliaji huyo kijana atapewa nafasi ya kung'aa kwenye kikosi cha kwanza hivi karibuni.
"Hapana, haendi tena kwa mkopo," Wenger aliwaambia waandishi wa habari baada ya mchezo wa nusu fainali katika ziara yao huko Asia. "Nilimpeleka kwa mkopo msimu uliopita maana niliamini ndicho aichokuwa akihitaji.
"Lakini msimu huu hapana, ninampango wakumuweka pamoja nasi. Inategemea na utendaji kazi na tabia na ana samani ya kuwa kipaji kikubwa. Na, baada ya hapo, kuwa mchezaji mwenye uwezo wiki baada ya wiki, hayo ndio malengo.
"Sasa inategemea na yeye. Kiasi gani sifahamu. Inampatia moyo kufanya vema na kuongeza juhudi zaidi. Ni mchezaji kijana na itamuongezea kujiamini. Namna ambavyo wachezaji wengine wanavyoonesha kujiamini ndani ya chumba cha kubadili nguo ni muhimu pia.
"Inaweza kukusaidia. Lakini tusisahau kuwa ni mechezo ya kirafiki. Ana kipaji kizuri lakini anapaswa kufanya kazi na kuonesha hicho katika kila mchezo."
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
BAADA YA KUTUPIA GOLI 3 "HAT-TRICK", WENGER AMPATIA NAFASI KIKOSI CHA KWANZA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment