
Baada ya klabu ya Liverpool kufikia makubaliano na klabu ya Aston Villa juu ya uhamisho wa mshambuliaji Christian Benteke, mchezaji huyo anategemea kufanyiwa vipimo vya afya.
Daktari wa kilabu hicho anatazamiwa kuelekea UK kutoka katika ziara ya timu hiyo huko Australia kukamilisha vipimo vya afya vya Benteke ndani ya masaa 48 yajayo.
Hata hivyo, mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 24 hatoungana na wechezaji wengine katika ziara hiyo.
Benteke alijiunga na Aston Villa akitokea Genk mwaka 2012 kwa ada ya pauni milioni 7, akifanikiwa kufunga magoli 49 katika michezo 101.
Baada ya kumuuza Raheem Sterling kwa wapinzani wao wa Ligi Kuu klabu ya Manchester City kwa ada ya pauni milioni 49, Liverpool iliamua kumnyatia mshambuliaji huyo.
Benteke, ambaye amebakiza miaka miwili katika mkataba wake na klabu ya Aston Villa, alifanikiwa kutupia magoli 12 katika michezo 12 msimu uliopita na kuisadia timu ya Tim Sherwood kutoshuka daraja.
Chanzo: Sport Football
Jumapili, 7/19/2015 09:57
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
CHRISTIAN BENTEKE KUFANYIWA VIPIMO VYA AFYA NDANI YA MASAA 48 YAJAYO...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment