PSG-DI MARIA:

Usajili wa winga wa klabu ya Manchester United Angel Di Maria ambae ndio chaguo la kwanza la kocha Laurent Blanc upo mbioni kukamilika kwa ada ya euro milioni 60.
Chanzo: Le Parisien
Jumanne, 7/14/2015 06:58
MAN CITY-BRUYNE:

Manchester City wameandaa dau la pauni milioni 35 ili kumnasa kiungo Kevin De Bruyne,japo wanapata ushindani toka kwa PSG na Bayern lakini bila shaka kiungo huyo atarejea Ligi ya Uingereza.
Chanzo: Daily Express
Jumanne, 7/14/2015 11:10
ROMA-DZEKO:

Klabu ya Manchester City imeiambia klabu ya Roma waongeze dau kufikia pauni 20 milioni ili kumpata mchezaji Edin Dzeko. Mratibu wa michezo wa kilabu hicho alipewa taarifa hizo alipokuwa Uingereza kwaajili ya kuzungumzia usajili wa mchezaji huyo.
Chanzo: talkSPORT
Jumanne, 7/14/2015 10:55
AJAX-SANOGO:

Mshambuliaji wa Arsenal Yaya Sanogo amekubali kujiunga na timu ya Ajax kwa mkopo wa muda mrefu.
Chanzo: De Telegraaf
Jumanne, 7/14/2015 00:25
MAN UTD-CAVANI:

Manchester United ipo kwenye mazungumzo na timu ya PSG juu ya kumnasa Edinson Cavan ila klabu hiyo ya Parc des Princes imeiomba Manchester United kumjumuisha Angel Dimaria kama sehemu ya malipo.
Chanzo: The Sun
Jumatatu, 7/13/2015 23:48
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
HABARI ZA USAJILI MAJUU...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment