
Meneja wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amempiga dongo mshambuliaji kutoka nchini Ureno pamoja na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo kwa kumtofautisha na kiungo mshambuliaji kutoka nchini Ubelgiji, Eden Hazard.
Mourinho ambaye yupo njiani kurejea nchini England sanjari na kikosi chake akitokea nchini Marekani walipokua wameweka kambi ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi, amesema Hazard ni mchezaji bora zaidi kuliko Ronaldo kutokana na uchunguzi wake alioufanya.
Meneja huyo kutoka nchini Ureno amesisitiza kuwa na uhakika wa jambo hilo ambalo alilizungumza mbele ya waandishi wa habari huko nchini Marekani huku akimuweka Ronaldo katika nafasi ya tatu kwa ubora duniani.
Alisema kwa soka la sasa ni vigumu kumfananisha Ronaldo na Hazard, hasa ikizingatiwa kiungo huyo wa klabu ya Chelsea msimu uliopita alikua lulu kwenye kikosi chake hadi kufikia hatua ya kutajwa kama mchezaji bora wa mwaka huko nchini England.
Mourinho, alikamilisha kwa kubainisha kwamba endapo akipewa nafasi ya kutaja walio bora duniani kwa sasa mchezaji wa kwanza kwake atakua Lionel Messi, kisha Eden Hazard halafu Ronaldo atafuatia.
Hata hivyo imekua ikiripotiwa kwamba Mourinho amekua hana mahusiano mazuri na Ronaldo wanapokua nje ya uwanja licha ya kuwahi kufanya kazi kwa pamoja huko mjini Madrid wakati meneja huyo alipokua mkuu wa benchi la ufundi la Real madrid.
Kabla ya Mourinho kwenda kukinoa kikosi cha Real Madrid, mara kadhaa aliwahi kumchokonoa Ronaldo kupitia vyombo vya habari lakini mshambuliaji huyo hakumjibu chochote zaidi ya kuendelea na shughuli zake za kucheza soka.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
HAZARD NI BORA KULIKO RONALDO-MOURINHO
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment