
Mashetani wekundu Man Utd, wameshindwa kufurukuta mbele ya mabingwa wa soka nchini Ufaransa PSG, baada ya kutandikwa bakora mbili kwa sifuri katika mchezo wa kujiandaa na msimu mpya wa ligi.
Man Utd ambao wamekua na mazingira mazuri ya kupata ushindi katika michezo yao ya kirafiki iliyopita, iliyochezwa huko nchini Marekani walijikuta wakilamba kisago hicho kufuatia uwezo mzuri ulioonyeshwa na wapinzani wao kutoka Ufaransa.
Mshambuliaji na nahodha wa timu ya taifa ya Sweden, Zlatan Ibrahimovic aliifungia PSG bao la pili katika dakika ya 34, baada ya kiungo kutoka nchini Ufaransa, Blaise Matuidi kufunga bao la kwanza katika dakika ya 25.
Katika mchezo huo mlinda mlango wa Man Utd, David De Gea alionekana kucheza chini ya kiwango na kocha wa Man Utd, Louis van Gaal alimtoa baada ya dakika 45 za kipindi cha kwanza.
Kutokana na hali hiyo, Van Gaal sasa anawaza mawili, amruhusu aende Real Madrid au ampe mkataba mwingine, lakini kizungumkuti kingine kinachomkabili meneja huyo kutoka nchini Uholanzi ni kuamini De Gea ana mtazamo chanya (uzoefu) katika kikosi chake kwa sasa.
David De Gea amekuwa akihusishwa sana kuhamia Real Madrid, ingawa uongozi wa Man Utd umekua ukiweka msimamo wa kutomruhusu kuondoka.
Mchezo huo wa kirafiki dhidi ya PSG umekua wa mwisho kwa mabingwa hao wa kihistoria katika soka la nchini England, na sasa watarejea nyumbani kumalizia sehemu ya maandalizi kabla ya kuanza kwa ligi mwishoni mwa juma lijalo.
Manchester United wataanza kurusha karata yao ya kwanza katika ligi ya nchini England dhidi ya Tottenham mnamo Agosti 8 mwaka huu.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
PSG YAICHAICHAPA MAN UNITED MBILI BILA...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment