
Mshambuliaji kutoka nchini Colombia, Jackson Arley Martínez, anaamini kusajiliwa kwake kwenye kikosi cha Atletico Madrid ni hatua nzuri kwa klabu hiyo ya mjini Madrid, kurejesha heshima ya kutwaa tena ubingwa wa nchini Hispania msimu ujao wa ligi.
Martinez, alieleza matarajio hayo, wakati aliposalimiana na mashabiki 10,000 waliokua wamejitokeza kwenye uwanja wa Vicente Calderón, katika shughuli ya kutambulishwa.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 28, amesema usajili wake anaamini utaongeza nguvu katika mipango ya klabu hiyo ya kuhakikisha wanarejesha heshima baada ya msimu uliopita kupokonywa ubingwa wa La Liga na FC Barcelona.
Hata hivyo amewataka mashabiki kuwa na uvumilivu pale mambo yatakapokwenda mrama katika msimu mpya wa ligi ya Hispania lakini akasisitiza wazi kwamba lengo ni mafanikio kwanza na mengine yatakayojitokeza katika safari yao yatachukuliwa kama majaribu.

Wakati wa shughuli ya kutambulishwa mbele ya mashabiki, baadhi ya makazi wa Atletico Madrid walishindwa kujizuia kwa furaha na kujikuta wakiruka uzio na kuingia kwenye sehemu ya kuchezea ili wakamilishe azma ya kumshika mshambuliaji huyo kitendo ambacho kilifanikiwa kabla ya maafisa wa usalama hawajawaondoa uwanjani.
Martinez, amejiunga na Atletico Madrid kwa usajili wa pauni milioni 25 akitokea FC Porto ya nchini Ureno.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
JACKSON ARLEY MARTINEZ ATAMBULISHWA RASMI ATLETICO MADRID...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment