
Kipa Sergio Romero, aliyekuwa akiichezea klabu ya Sampdoria, amejiunga na vijana wa Louis Van Gaal baada ya kukamilisha muda wa mkataba wake na Sampdoria.
Romero aliwahi kucheza chini ya Van Gaal katika timu ya AZ Alkmaar ya Uholanzi iliyotwaa ubingwa wa kombe la ligi ya Uholanzi mnamo mwaka wa 2009.
Kipa huyo ametia saini mkataba wa miaka mitatu na anatarajiwa kuchukua nafasi ya kipa wa akiba, Victor Valdes ambaye ameambiwa yuko huru kuihama klabu hiyo na Van Gaal.
Romero alikuwa katika timu ya taifa ya Argentina iliyofika fainali ya Copa America mwaka huu na kombe la dunia nchini Brazil mwaka uliopita.
Kwa sasa kipa huyo ameungana na wana-devils katika kambi ya mazoezi ya timu hiyo nchini Marekani.
Mchezaji huyo ni miongoni mwa wachezaji waliofunzwa na Van Gaal ambao wameungana naye Old Trafford wengine wakiwa ni Memphis Depay, na Daley Blind.
Hatua ya kumsaini Romero inaonekana ni kama njia ya kupiga jeki idara ya ulinzi katika Manchester United huku Mhispania, David De Gea akiendelea kusakwa na Real Madrid.
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
MAN UTD YAMSAJILI KIPA SERGIO ROMERO...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment