CHELSEA-PEDRO:

Mchezaji wa klabu ya Barcelona Pedro Rodriguez amekubali kujiunga na klabu ya Chelsea baada ya kufanya mazungumzo ya simu na meneja wa klabu hiyo Jose Mourinho na Cesc Fabregas alimshauri mshambuliaji huyo kutua Chelsea ambao walikuwa Mabingwa wa Ligi msimu uliopita.
Chanzo: Sport
Jumapili, 7/12/2015 08:13
MAN UTD-BENTEKE:

Kocha wa Manchester United Louis van Gaal amefanya usajili wa mshambuliaji kuwa muhimu zaidi na amepanga kumsajili mshambuliaji wa Aston Villa Christian Benteke.
Chanzo: The Sun
Jumapili, 7/12/2015 07:15
EVERTON, ASTON VILLA, CRYSTAL PALACE-JORDAN AYEW:

Timu tatu kutoka Uingereza Everton, Aston Villa na Crystal Palace zinamuwania mshambuliaji wa klabu ya Lorient Jordan Ayew. Klabu ya Lille imehusishwa pia na nia ya kumsajili mshambuliaji huyo lakini huenda wakashindwa kumsajili kutokana na bei yake kuwa kubwa kutokana na timu za Uingereza kumuwania.
Chanzo: L'Equipe
Jumapili, 7/12/2015 08:40
ROMA-DZEKO:

Roma imekubaliana na klabu ya Manchester City kuhusiana na usajili wa Edin Dzeko. Mshambuliaji huyo ataelekea Serie A kwa mkopo lakini Roma watakuwa na uchaguzi wa kumsajili kwa ada ya euro milioni 20 (£14.3m).
Chanzo: La Repubblica
Jumapili, 7/12/2015 08:36
MAN UTD-RAMOS AND NAVAS:

Klabu ya Manchester Utd imeiambia klabu ya Real Madrid kuwajumuisha wachezaji Sergio Ramos pamoja na Keylor Navas kwenye dili lao la kumsajili mlinda mlango David De Gea.
Chanzo: Marca
Jumapili, 7/12/2015 07:45
ARSENAL-MANOLAS:

Klabu ya Arsenal imeamsha tena matamanio yao ya kumsajili mlinzi wa kati wa klabu ya Roma Kostas Manolas. Beki wa kati wa Manchester United Jonny Evans pia amehusishwa na kujiunga na washika bunduki hao wa Londoni.
Chanzo: Daily Star
Jumapili, 7/12/2015 07:45
MAN CITY-STERLING:

Manchester City wamewasilisha dau la tatu kwa klabu ya Liverpool lenye thamani ya pauni milioni 40 kwa ajili ya kumnasa winga wa klabu hiyo Raheem Sterling.
Chanzo: The Sun
Jumapili, 7/12/2015 07:13
Firmino atua Liverpool
Klabu ya Liverpool imekamilisha usajili wa mchezaji wa Hoffenheim Roberto Firmino kwa ada isiyofahamika, huku akitegemea kufanyiwa vipimo vya afya. Mkurugenzi wa Liverpool Ian Ayre alielekea Chile kwa ndege, ambako Firmino anashiriki mashindano ya Copa America ili kumalizia usajili huo unaosadikika kuwa umegharimu euro milioni 40. Baada ya mashindano hayo kumalizika, mchezaji huyo atafanyiwa vipimo vya afya.
Jara aoneshwa mlango wa kutokea baada ya kuchafua hewa
Baada ya kumfanyia mambo machafu mchezaji wa Uruguay Edinson Cavani, mchezaji wa klabu ya Mainz Gonzalo Jara ameambiwa na klabu yake kuwa haitovumilia kitendo hicho na anaweza kutimka klabuni hapo mara tu ofa yoyote itakapopatikana.
Real Madrid yakataa ofa ya Man Utd
Real Madrid wametaa dau la kwanza lililotolewa na klabu ya Manchester Utd kwa ajili ya kumpata beki wa kati wa klabu hiyo Sergio Ramos. Miamba hiyo ya Hispania imepanga kumuuza beki huyo kwa dau la pauni milioni 64 na haitahusisha usajili wa kipa David De Gea kama klabu ya Manchester Utd ilivyokuwa ikihitaji.
Pogba kutua Man City kabla ya Sterling
Manchester City wanataraji kukamilisha usajili wa kiungo mfaransa Paul Pogba. Usajili huo unatazamiwa kukamilika hata kabla ya usajili wa winga wa Liverpool Raheem Sterling.
Cech ndani, Ospina nje Arsenal
Klabu ya Arsenal inaweza kumuuza golikipa wake David Ospina licha ya kufanya vema mzunguko wa pili wa msimu uliopita. Klabu ya Fenerbahce imeonesha nia kubwa ya kumuwania kipa huyo huku kipa aliyeonekana kusuasua mara kwa mara Wojciech Szczesny akitegemewa kuwa msaidizi wa Petr Cech.
PEDRO AMEKUBALI KUTUA CHELSEA, BENTEKE KUTUA MAN UTD, ARSENAL IMEREJEA TENA KWA MANOLAS...
Popular Posts
-
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid Ramon Calderon anafikiria kuwa klabu ya Manchester United itakuwa imetumia hekima kumsajili Ser...
-
ARSENAL INA MATUMAINI YA KUMNASA BENZEMA: Azma ya Arsenal kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema imepata mwamko mpya baada ...
-
KIIZA APEWA WIKI MBILI KUONGEZA KIWANGO
-
Chile imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya Copa America baada ya kuichapa Uruguay 1-0, lakini mapema kipindi cha pili mshambuliaji...








0 comments:
Post a Comment